Tuesday, September 11, 2012

Waalimu wa Idara Yangu, Chuoni St. Olaf

Hapa ni picha iliyopigwa siku chache zilizopita ya walimu wa idara ya ki-Ingereza katika Chuo cha St. Olaf. Nimefundisha katika idara hii tangu mwaka 1991. Kuanzia mwaka 1976 hadi huo mwaka 1991 nilikuwa mwalimu katika idara ya Literature, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Chuo cha St. Olaf kinatoa shahada ya kwanza katika masomo mbali mbali.

Walimu wengi niliowakuta katika idara hii hapa St. Olaf wamestaafu. Waliobaki, ambao wamo pichani, ni watano tu, na mwingine, wa sita, hayupo katika picha hii. Nimekuwa mwalimu pekee kutoka Afrika tangu ule mwaka 1991, na sasa nami nimeanza kuwazia suala la kustaafu, ili nirudi Tanzania nikiwa bado na umri wa kuendelea na kazi za taaluma.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...