Friday, March 1, 2013

Yatokanayo na Mhadhara Wangu Mjini Faribault

Sikupenda kuelezea kirefu mafanikio ya mhadhara niliotoa katika chuo cha South Central, mjini Faribault kwa wanafunzi na maprofesa wanaojiandaa kwa safari ya Afrika Kusini. Niligusia tu kuwa mhadhara ulikuwa mzuri. Undani wa kilichotokea ni habari ambayo nataka niwaachie waliohudhuria waelezee.

 Kwenye ukurasa wa Facebook, Profesa Becky Davis aliweka picha ambayo nimeiazima hapa, na pia aliandika hivi:

Joseph Mbele spoke with us this morning. What a generous spirit, and what a delightful and humorous speaker!

 Kwa upande wangu, mihadhara ya aina hii ninaitoa mara kwa mara, kwenye vyuo, taasisi na jumuia mbali mbali hapa Marekani. Msingi wake ni yale niliyoandika katika kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Mialiko hii inatoka zaidi kwa waMarekani ambao wanapangia safari ya Afrika au wanashughulika kwa namna mmoja au nyingine na waAfrika, iwe ni barani Afrika au hapa hapa Marekani.

Watu hao, ambao ni wengi sana, wakishasoma kitabu hiki wanapata hamasa ya kunialika nikaongelee masuala husika na hapo tunapata fursa ya kwenda ndani na mbali zaidi ya pale nilipofikia katika maelezo yangu kitabuni. Nimewaheshimu wa-Marekani hao,  kwa ari yao ya kujielimisha kuhusu tofauti za tamaduni kama njia ya kuboresha mahusiano na pia kujihakikishia mafanikio katika shughuli zinazowajumuisha na tamaduni tofauti.

Napenda nimalizie kwa kutoa ujumbe kwa wengine. Kila ninapopata mwaliko wa kutoa mihadhara hiyo, nahikikisha nimejizatiti ipasavyo ili kutoa mchango wa kiwango cha juu. Kwa namna hiyo, nawapa faida wahusika, na kisha wao wanakuwa wapiga debe wangu. Msingi mkuu wa mafanikio ni juhudi na umakini.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...