Monday, December 2, 2013

Ninayo Pia Blogu ya Ki-Ingereza, Jamani

Wadau wa blogu hii ya hapakwetu, samahani kama sikuweka wazi tangu mwanzo kuwa ninayo pia blogu ya ki-Ingereza. Inaitwa "Mbele" na anwani yake ni hii: http://www.josephmbele.blogspot.com.

Niliamua kuanzisha na kuendesha blogu hii ya ki-Kiingereza ili kuchangia elimu hasa katika masuala ya fasihi ya ki-Ingereza. Mimi ni mwalimu wa somo hili mwenye uzoefu tangu miaka ya mwanzoni ya sabini na kitu. Nilifundisha katika idara ya Literature, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuanzia mwaka 1976, nikasomea shahada ya udaktari Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison, Marekani, 1980-86, na kuanzia mwaka 1991 nimekuwa nikifundisha katika idara ya ki-Ingereza ya chuo cha St. Olaf hapa Marekani.

Katika blogu hii ya "Mbele" mara kwa mara ninaongelea vitabu, hasa vitabu vya fasihi. Uchambuzi wangu vitabu hivi unasomwa duniani kote. Nimeona kuwa uchambuzi wangu wa riwaya ya The Old Man and the Medal unapitiwa kuliko andiko jingine lolote na watu kutoka duniani kota.

Nina uzoefu na ufahamu mkubwa sana katika masomo hayo, na ndio nikaona niwamegee wanajamii angalau kiasi, kwani blogu si mahala pa kuandika makala ndefu, wala kitabu. Nilivyoanzisha blogu hii ya ki-Ingereza niliwawazia kwa namna ya pekee vijana wa Tanzania.

Nikiongea kwa ujumla kuhusu wa-Tanzania, ni kwamba wale wanaodhani wanajua ki-Ingereza, bado wana safari ndefu. Mimi mwenyewe naendelea kujifunza undani wa ki-Ingereza, ingawa waandishi maarufu hapa Marekani kama vile Mzee Patrick Hemingway na Jim Heynen wanapenda ninavyoandika. Ni jambo baya sana kuridhika na kile unachodhani unajua, na ndio maana nafanya juhudi.

Ninaandika ki-Ingereza sahihi, ipasavyo, na nilitegemea kuwa yoyote anayeisoma blogu ya Mbele kwa makini ataona mfano wa uandishi bora wa ki-Ingereza. Ninafahamu ninachosema, kwani kama nilivyotamka, mimi nafundisha ki-Ingereza katika chuo hapa Marekani. Lakini bado nahangaika kuboresha ujuzi wangu kwa kusoma sana na kuandika sana.

Nimeandika ujumbe huu kwa sababu mbili zinazohusiana. Hutokea mara moja moja mdau akaniuliza blogu yangu nyingine anwani yake ni ipi. Pili, nimegundua kuwa kuitaja tu katika orodha ya blogu niliyoweka hapa kulia, haitoshi. Soma pia makala hii hapa.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...