Friday, May 9, 2014

Kitabu Kinawasaidia Wasafiri waMarekani

Ni furaha kwangu ninapoona malengo niliyokuwa nayo katika kuandika kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences yanaendelea kutimia. Lengo kubwa lilikuwa kuwasaidia Wamarekani kuufahamu utamaduni wa MwAfrika, kadhalika kuwasaidia waAfrika kuufahamu utamaduni wa waMarekani.

WaMarekani wana tabia ya kusoma kuhusu nchi waendako. Nimeshaona tena na tena jinsi wale waendao Afrika wanavyosoma kitabu changu hicho Kama sehemu ya maandalizi ya safari.

Jana, wakati navinjari mtandaoni, niliona taarifa kutoka kwa wasasfiri kutoka Wisconsin ambao walienda Tanzania hivi karibuni. Kwa vile walishasoma kijitabu changu kabla ya kusfiri, ilikuwa rahisi kwao kuelewa mambo walioyoyaona kule Tanzania. Katika taarifa yao wameandika hivi:

In the United States we are accustomed to running from place to place, chasing time and cramming all we can into a day. In Tanzania we found a slower pace--we experienced "African Time." The day is not driven by the clock but rather shaped by people's relationships. It is accepted practice to be "late" as a result of lending a helping hand, catching up with an old friend, or extending hospitality to a stranger. This is something we learned prior to landing at the Julius Nyerere International Airport, having read "Africans and Americans: Embracing Cultural Differences" by Joseph L. Mbele as part of our seminar pre-work.

Kifungu hiki nimekinukuu kutoka katika taarifa nzima, ambayo ni hii hapa:www.leadershipwisconsin.org/2014/04/24/safari-of-a-lifetime-part-I/.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...