Wednesday, May 14, 2014

Nimejifunza Katika Kuwapiga Picha Ndege

Nimejifunza mambo kadhaa katika kuwapiga picha ndege  kiasi cha yadi chache tu kutoka hapa nyumbani.

Kwanza sio ndege wa aina zote wanaruka zao  ukijaribu kuwasogea. Kuna aina ya ndege ambao  wana subira. Hao ni rahisi kuwapiga picha.

Katika ujumbe wangu wa juzi, sikufafanua suala hilo. Kwa hivi, leo narekebisha kauli yangu.


Jambo jingine ambalo nimejifunza ni kuhusu matumizi ya "zoom" kwenye kamera. "Zoom" ikielekezwa kwa ndege peke yake, halafu akakuzwa sana bila kitu kingine pembeni,  inapotosha ukubwa au udogo halisi wa ndege huyu. Ndege mdogo kabisa anaweza kuonekana mkubwa kama kuku.

Kwa hiyo leo nimejaribu kuwaonesha ndege wakiwa katika mazingira yao ili ukubwa au udogo wao ufananishwe na nyasi zinazowazunguka, au majani, au vijiti.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...