Monday, May 12, 2014

Ndege Mhandisi

Leo, katika matembezi huko nje, nilimwona ndege huyu akiwa ardhini, sio mtini. Alikuwa ng'ambo ya barabara, name nikiwa ng'ambo ya pili.

Kwa macho, alionekana ndege mdogo. Lakini nilipompiga picha, nikiwa nimefungua "zoom" ya kamera, nimegundua kuwa alikuwa amebeba nyasi mdomoni. Bila shaka ni nyasi za kujengea kiota.

Nilivutiwa na jinsi ndege huyo alivyo na nidhamu. Alifanya kazi hiyo bila usimamizi au amri ya yeyote. Na aliifanya kwa uaminifu ina kujiamini. Laiti wanadamu wote tungekuwa na moyo wa aina hii.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...