Saturday, August 2, 2014

Tamasha la Afrifest Limefana

Tamasha la Afrifest 2014 lilifanyika jana na leo hapa Minnesota. Jana jioni, shughuli ikuwa ni maonesho ya mavazi na muziki, kama inavyoonekana katika tangazo hapa kushoto.

Sikuweza kuhudhuria shughuli za jana, kutokana na masuala ya matibabu, lakini leo nimejikongoja hadi Brooklyn Park, ambako shughuli ya leo ilifanyika. Kule nilipata taarifa za mambo ya jana, kwamba yalifanikiwa vizuri kabisa.

Leo niliweza kwenda kuhudhuria Brooklyn Park ambako shughuli ziliendelea, kama ilivyopangwa. Nilikuwa pamoja na binti zangu, Assumpta na Zawadi.
Kama kawaida, watu kutoka nchi mbali mbali za Afrrika, Marekani, na kwingineko walihudhuria.

Kulikuwa na maonesho ya vitu  mbali mbali, kuanzia mavazi, vitu vya urembo, vitabu na machapisho mengine. Vile vile vile walikuwepo wauza vyakula.

Benki ya Wells Fargo. ambayo sasa huhudhuria Afrifest kila mwaka, ilikuwa na banda lake, ambapo paliwekwa taarifa za huduma za benki hiyo, na watu walikuwa na fursa ya kujiunga kama wateja.

Ilipokaribia jioni, kulikuwa na shindano la soka baina ya Afrika Mashariki na Magharibi, ambalo lilileta msisimko. Kama ilivyokuwa miaka iliyopita, tamasha la Afrifest la leo lilitoa fursa kwa watu kuja na kuondoka walivyopenda. Wengine walikuja hiyo jioni, kuangalia hayo mashindano ya soka. Sikukaa sana kiasi cha kuweza kuangalia mashindano hayo, ila niliona wachezaji walipokusanyika uwanjani.

Kitu kimoja cha pekee mwaka huu ni banda ambalo lilikuwa sehemu ya kukusanyia michango ya vitu mbali mbali kwa ajili ya waathirika wa ugonjwa wa ebola nchini Liberia na sehemu zingine za Afrika Magharibi.

Kwa upande wangu, niliweza kuongea na watu wengi waliofika kwenye meza yangu. Walitaka kujua mambo ya aina mbali mbali. Kwa mfano baadhi walitaka kujua mtazamo wangu kuhusu mahusiano baina ya wa-Afrika na wa-Marekani Weusi. Nilitamka wazi kuwa kuna changamoto nyingi na inahitajika elimu ya dhati na endelevu  kwa pande zote, kama tuna nia ya kujenga maelewano sahihi na mshikamano. 

Wengi, kama ilivyo kawaida, walitaka kufahamu kuhusu shughuli zangu, na hasa maandishi yangu. Nilipata fursa ya kujieleza kwa hao watu mbali mbali. Baadhi walinunua vitabu. Vile vile, nilihojiwa na kituo kimoja cha televisheni.

Hapa naleta picha kadhaa, zinazohusiana na  yale niliyosema hapa juu.














No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...