Saturday, October 13, 2018

Nimeshiriki Tamasha la Vitabu la Deep Valley

Leo nilienda Mankato, Minnesota, kushiriki tamasha la vitabu liitwalo Deep Valley Book Festival. Hii ilikuwa mara yangu ya nne kushiriki tamasha hilo. Ilikuwa fursa ya kuongea na watu kwa undani kuhusu mambo mbali mbali.

Kuna watu kadhaa ambao nawakumbuka zaidi. Mmoja aliniambia kuwa ana binti yake ambaye anafundisha ki-Ingereza kama lugha ya kigeni. Hapa Marekani somo hilo linajulikana kama English as a Foreign Language. Hufundishwa kwa wahamiaji ambao wanahijtaji kujia lugha hiyo, ambayo ndio lugha rasmi ya hapa Marekani. Nilichangia mada hiyo kwa kuelezea jinsi sgughuli ya kufundisha ESL inavyofungamana na suala la tamaduni. Hufundishi tu muuno, sarufi, istilahi, bali pia utamaduni wa mazungumzo.

Mama mmoja mzee, mwandishi, ambaye meza yake ilikuwa mbele yangu, alifika kunisalimia na kuongea. Nilimwuliza ameandika kuhusu nini, akaniambia kitabu chake kinahusu changamoto aliyopitita kufuatia binti yake kujitokeza kama mwenye silika ya mapenzi ya jinsia yake. Nilivyomwelewa huyu mama, ilikuwa ni changamoto kubwa kwake, na ndiyo aliyoandika kitabuni. Nilimwambia kuwa nami nilianza kuelewa suala hili la mapenzi ya jinsia moja nilipokuwa masomoni katika chuo kikuu cha Wisconsin-Madison, ambapo palikuwa na wana harakati wa aina mbali mbali. Nina nia ya dhati ya kukipata ta kiabu chake.

Kijana mmoja alikuja mezani pangu akaniambia kuwa anafuatilia habari za mwandishi Sinclair Lewis. Anamwigiza, yaani kujifanya yeye ndiye mwandishi huyo. Akaniuliza iwapo ataweza kupata wapi habari zaidi. Nikamwambia kuwa kwa bahati nzuri, Marekani ni Makini kwa kutunza taarifa za watu mashuhuri kama hao waandishi. Nilimwabia kuhus nyumba ya makumbusho ya Carl Sandburg, ambayo niliwahi kuitembelea, mjini, Galesburg, Illinois, na nyumba za makumbusho ya Ernest Hemingway ambayo niliwahi kutembelea mjini Oak Park, Illinois, na sehemu zingine, kama vile maktaba ya JF Kennedy ambayo niliwahi kuitembelea Boston.

Watu wamenieleza uzoefu wao wa kuishi na waAfrika hapa Marekani na kujione tofauti za tamaduni, kwa maana ya mienendo, namna ya kufikiri na kutenda. Mzee moja aliniambia kuwa ana jirani mSomali. Alinunua kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, nami nikamhimiza asikose kumwazimisha huyu mSomali asome.

Nami nimepata fursa ya kuwaeleza wat hao kuhu mialiko ninayopata kwenda sehemu mbali mbali kuelezea athari za tofauuti za tamaduni. Wakati wa kuongelea kitabu changu, nimeelezea mtindo wa uandishi niliotumia. Nimepata fursa ya kuongelea kitabu cha Matengo Folktales, pia, nilivyokiandaa kwa miaka mingi, tangu kurekodi hadithi hadi kuzitafsiri na kuzichambua, na hatimaye kuchapishwa. Sikukosa kuelezea kilivyotajwa mwezi November tarehe 23 katika kipindi cha TV ch Jeopardy. Nilikuwa nimechukua karatasi yenye tamko la Jeopardy a, ambao  hawakuweza kujibu/.

Mbali ya vitabu vyangu, nilichukua vitabu vya Bukola Oriola na kitabu cha mwanae Samuel Jacobs, mwenye umri wa miaka kumi na moja. Bukola Oriola niliwahi kumzungumzia katika blogu hii. Tangu nilipomwelekeza namna ya kuchapisha kitabu chake cha kwanza, amefika mbali. kwani aliteuliwa na Rais Obama kuwa katika United States Advisory Council on Human Trafficking.

Nimekutana na rafiki yangu Becky Fjelland Brooks, mwalimu wa South Central College, ambaye ni mpenzi mkubwa wa kitabu changu cha Africans and Americans, amewahi kunikalika mara kadhaa nikaongee na wanachuo wake. Akaandika taarifakadhaa, kama hii hapa na hii hapa.


No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...