Sikujua kama ningekikuta, kwani sijui utaratibu wanaofuata katika kuvionesha vitabu hivyo sehemu hiyo. Nilidhani labda vinawekwa kwenye kabati hili kwa wiki moja hivi. Nilishangaa kukiona kitabu changu bado kipo, na kimewekwa juu zaidi ya pale kilipokuwepo kabla. Hapa kushoto ni picha niliyopiga wiki iliyopita, na kulia ni picha niliyopiga juzi. Ninafarijika na kufurahi kukiona hapa. Ninasubiri siku ya kwenda kukiongelea, kama nilivyodokeza.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjFXaDmDUu4U16cOXwMsFqiQxCbG0onO5Kh8fqoZSeU7B9MLnEHiKbCpnue0EwlEV2PYxwA8gxJG_Y_NygI2GJR00-qMOjkoJoUa6GZiT-Ufdc0PLJz641fVzW8zNSj_QRWtMOTfIa297s/s320/42415436_10204669301289285_8172463062159196160_n.jpg)
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiZDNVKNgXY0hLJqn3hgAhsu5FZKPC1fppmysIfxcNgJUKjx1a4dlJ0mUeZ2hagBKJh1dA7KaTzDeqI-0pH5WNFhkh6V_YDZH2h_XQROQSl3t_lbzPiPQYu35VnZIFBWlHWulczk83_wmg/s320/44167151_10204744558050657_1016872853523398656_n.jpg)
No comments:
Post a Comment