Sunday, September 25, 2022

Mkutano na Mmiliki wa African Travel Seminars

Tarehe 22 Septemba, nilikutana na Georgina Martin Lorencz, mmiliki wa African Travel Seminars, kampuni ya utalii inayopeleka watu sehemu mbali mbali duniani. Huyu mama mwenye asili ya Ghana tunafanana kimtazamo kuhusu utalii. Tunataka utalii unaolinda heshima na utu, unaoboresha maelewano, na usio na hali yoyote ya udhalilishaji na ukoloni mamboleo. Tunataka manufaa ya utalii yaonekane katika jamii inayofikiwa na watalii.

Zaidi ya hayo, Georgina  ni kati ya wale wanaotumia kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences katika shughuli zao. Kuafiki kwao yale ninayosema kuhusu utamaduni wa waAfrika kunsnifanya nijisikie vizuri. Hiyo juzi nilimkabidhi kitabu changu kipya, Chickens in the Bus: More Thoughts on Cultural Differences.

Kuna mambo muhimu tumepangia kufanya, ikiwemo kufungua njia mpya za utalii Tanzania, kuongezea programu iliyopo Tanzania ya African Travel Seminars. Taarifa zitapatikana kadiri muda unavyokwenda. 

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...