Showing posts with label Iringa. Lutheran College Consortium for Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Iringa. Lutheran College Consortium for Tanzania. Show all posts

Wednesday, May 11, 2011

Nimekutana na Mpiga Debe Wangu

Leo nimekutana na mzee Don Fultz na Mama Eunice Fultz katika mji wa Eagan, Minnesota. Nilienda kule na mfanyakazi mwenzangu wa chuo cha St. Olaf ambaye tunashughulikia programu za kupeleka wanafunzi nchi za nje. Katika picha hizi, Mzee Fultz na Mama Fultz wameketi katikati.

Mzee Fultz ni mchungaji wa kanisa la ki-Luteri, sinodi ya St. Paul. Anaishi hapa Minnesota na Iringa, akiendesha programu za ushirikiano.

Mchungaji Fultz ni mtu wa pekee kwangu. Ni mfuatiliaji makini wa shughuli zangu za kuwaelimisha wa-Marekani na wa-Afrika kuhusu tofauti za tamaduni zao. Ni mpiga debe mkubwa wa kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.

Tangu wakati kitabu hicho kilipokuwa ni kijimswada tu kisichokamilika, Mchungaji Fultz alikibeba na kukipigia debe hapa Marekani. Hakuwa peke yake katika kufanya hivyo. Nilivyoona hivyo nilishtuka, nikaamua kukifanyia kazi kimswada hiki na kukiboresha.

Kazi hiyo niliifanya kila siku kwa miezi minne, hadi nikakichapisha kitabu mwezi Februari 2005. Mchungaji Fultz alikiandikia makala kwenye kijarida cha kanisa mojawapo hapa Minnesota, mbali na kuendelea kukipigia debe kwenye mikutano mbali mbali na kwa watu binafsi katika maandalizi ya safari za Tanzania. Wa-Marekani wengi wameniambia kuwa walisikia habari za kitabu hiki kutoka kwake. Wengine wamewapelekea nakala wa-Tanzania.

Leo tulikutana kuongelea mambo ya Iringa, kwani ninapangia kuwepo kule kwa wiki mbili mwaka huu na wanafunzi katika programu ya LCCT ambayo ni ya ushirikiano na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Ingawa Iringa niliifahamu vizuri zamani, nimejifunza mengi kutoka kwa Mzee na Mama Fultz kuhusu Iringa ya leo.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...