Showing posts with label Tarangire. Show all posts
Showing posts with label Tarangire. Show all posts

Friday, May 30, 2014

Tembo wa Hifadhi ya Tarangire, Tanzania

Tarangire ni moja ya hifadhi maarufu Tanzania, yenye wanyama mbali mbali.

Nimefika katika hifadhi hii mara nne, kwa miaka tofauti. Mwezi Januari, mwaka juzi, 2013, nilipiga picha mbali mbali. Baadhi ni picha za tembo zinazoonekana hapa. Nilikuwa naongoza darasa la wanafunzi 29 wa chuo cha St. Olaf, katika kozi ambayo nilikuwa nimeitunga, kumhusu Ernest Hemingway.





Mwandishi Ernest Hemingway aliitembelea hifadhi hii mwaka 1933. Aliandika hayo katika kitabu chake cha Green Hills of Africa ambamo amezitaja na kuzielezea sehemu nyingi za Tanganyika alimopita.

Green Hills of Africa, kwa mtazamo wangu, ni kitabu bora sana, ambacho kiliitangaza nchi yetu vizuri kabisa, kuliko ambavyo sisi wenyewe tumefanya, kuliko tunavyoweza. tunaendekeza uzembe katika lugha na katika nidhamu ya uandishi kama ille ya Hemingway.. 



Kila ninapofika sehemu kama Tarangire, ninamkumbuka Hemingway na maandishi yake, hasa hiki kitabu chake cha Green Hills of Africa. Haiwezekani kujizuia.

Thursday, May 29, 2014

Duka Dogo Langoni pa Hifadhi ya Tarangire

Mwezi Januari, mwaka 2013, nilikuwa nazunguka maeneo ya kaskazini mwa Tanzania na wanafunzi 29 wa chuo cha St. Olaf. Tulikuwa katika kozi kuhusu safari za mwandishi Ernest Hemingway, tukisoma maandishi aliyoandika kuhusu sehemu hizo. Kati ya sehemu tulizotembelea ni hifadhi za Ngorongoro, Serengeti, Manyara, na Tarangire.

Kwenye sehemu ya kuingilia Tarangire, niliona duka dogo ambalo lilinivutia. Niliamua kupiga picha.



 


Kwa wale ambao wamefika Tarangire, hapa mahali ni karibu kabisa na Tarangire Safari Lodge. Ingawa nilishafika Tarangire mara mbili tatu miaka iliyotangulia, sikumbuki kama nililiona duka hili. Nilivutiwa na rangi mbali mbali za vitu vilivyokuwa vinauzwa humo. Nilijisikia kama vile naangalia kazi ya sanaa.

















Kwa wale ambao hawajafika, nimeona ni jambo jema kuwapa fununu kidogo kuhusu vitu ambavyo vinanivutia nchini mwetu.










Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...