Saturday, August 25, 2012

Mwanaanga Neil Armstrong Amefariki

Mwanaanga Neil Armstrong alikuwa binadamu wa kwanza kutua na kutembea mwezini, Julai 20, 1969. Dunia nzima ilisisimka kutokana na tukio hilo. Wakati ule nilikuwa shuleni, kidato cha tatu.

Tulifuatilia kwa makini habari nzima za shirika la NASA hadi kufikia hatua ile ya kihistoria. Hayo nayakumbuka vizuri sana. Nakumbuka pia kuwa sheikh moja wa Tanzania alitoa tamko kuwa haiwezekani binadamu kwenda mwezini, kwani Quran haiafiki.

Kwetu sisi, Neil Armstrong alikuwa shujaa, pamoja na wenzake Edwin Aldrin na Michael Collins waliosafiri naye kwenye chombo chao, Apollo 11. Nakumbuka kuwa katika Tanzania, kuna watu waliviita vyombo vyao vya usafiri, kama vile magari, Apolo 11.

Neil Armstrong amefariki, akiwa na umri wa miaka 82. Mungu amweke mahali pema Peponi. Amina.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...