Thursday, August 23, 2012

Utamaduni wa Kusoma Vitabu

Picha hii nimeiona kwenye mtandao wa VOA NEWS. Ilipigwa ufukweni Ziwa Nyasa, upande wa Malawi.

Nimevutiwa na huyu mtalii anayejisomea kitabu. Ninafahamu manufaa ya kusoma vitabu; navisoma kila siku. Nafahamu faida ya kuwa na vitabu, kwani ninavyo zaidi ya 3000.

Kama ninavyoandika mara kwa mara katika blogu hii na sehemu zingine, utamaduni wa kusoma vitabu uko sana miongoni mwa wa-Marekani. Ni kawaida kwa wa-Marekani kuwanunulia wenzao vitabu kama zawadi, kwa mfano kwenye nyakati muhimu kama Krismasi.

Wa-Marekani wanapokwenda nchi yoyote kama watalii, ni kawaida kwao kutafuta vitabu kuhusu nchi ile, wavisome kabla ya kusafiri, wakishafika kwenye nchi ile, au wakisharudi kwao. Ndio maana watalii hao hupenda sehemu zenye maduka ya vitabu.

Wa-Tanzania wangekuwa makini wangetambua na kuitumia fursa hiyo, kama nilivyoelezea katika kitabu cha CHANGAMOTO: Insha za Jamii. Lakini lazima nikubali kuwa kuweka mawazo na mawaidha katika kitabu haiisaidii jamii ambayo haina utamaduni wa kusoma vitabu.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...