Thursday, August 30, 2012

Uzinduzi wa Mzunguko wa Tano wa Mashindano ya Uandishi





 Mwenyekiti wa Bodi ya Mradi wa Vitabu vya Watoto Tanzania (CBP), Abdullah Saiwaad (kushoto), akimkabidhi Mkama Mwijarubi, hundi ya dola za kimarekani 2000 Dar es Salaam jana, baada ya kitabu chake alichoandika cha Kiss Kiddo: The birthday party kuchaguliwa kuwa moja ya kitabu bora ambacho kitaingia katika mzunguko wa nne wa mashindano ya uandishi wa riwaya za kiingereza kwa ajili ya vijana. Katikati ni Katibu Mtendaji wa Mradi huo Pilli Dumea.
Katibu Mtendaji wa Mradi wa Vitabu vya Watoto Tanzania (CBP), Pilli Dumea (katikati), akiwaonesha waandishi wa habari Dar es Salaam jana, moja ya vitabu vilivyo ingizwa katika muhutasari wa vitabu bora vilivyoandikwa kwa lugha ya kiingereza chini ya mradi huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya (CBP), Abdullah Saiwaad na Mwenyekiti wa Kamati ya Ushauri ya Tuzo ya Burt Adam Shaffi.
--
Na Mwandishi Wetu
Tuzo ya Burt ya Fasihi ya Kiafrika ni Mradi ulioanzishwa na Shirika la Kimataifa la Elimu, CODE kwa ufadhili wa Bwana Bill Burts ambaye ni Mkanada.
Madhumuni makubwa ya Mradi huu ni kuwezesha upatikanaji wa vitabu vya kujisomea vitakavyowasaidia wanafunzi walioko katika shule za msingi kujifunza Kiingereza ili kujiandaa kwa elimu ya sekondari ambayo inatolewa kwa Kiingereza.
Aidha vitabu hivyo vinalenga katika kuhamasisha usomaji miongoni kwa vijana, pamoja na kukuza uchapishaji na fasihi ya Kiafrika. Zaidi ya hayo, Mradi unalenga katika kutambua waandishi bora wa Afrika na vitabu bora kutoka Afrika.
Hadi  sasa Mradi umeweza kuchapisha vitabu aina 9 ambavyo ni:
1.      Tree land: The Land of Laughter
2.      The Best is Yet to Come
3.       A Hero’s Magic
4.      Face Under the Sea
5.      Living in the Shade
6.      In the Belly of Dar es Salaam
7.      Close Calls
8.      Lesssilie the City Maasai
9.      The Choice
Miswada bora ya mzunguko wa nne ni:
1.      Run Free - Richard Mabala
2.      Tears From Lonely Heart - Israeli Yohana
3.      Kiss Kiddo: The birthday party - Mkama Mwijarubi.
Hivi sasa miswada hiyo inachapishwa na wachapishaji waliowasilisha miswada hii ambao ni: E& D Vision Publishing, Mkuki na Nyota na Aidan Publishing
Mashindano ya mzunguko wa tano yataanza leo tarehe 29 Agosti, 2012 hadi Machi, 30, 2013, ambapo wachapishaji watatakiwa kuwasilisha miswada yao katika ofisi za Mradi.
Mafaniko ya Tuzo ya Burt ya Fasihi  ya Kiafrika
1.      Tuzo ya Burt imeweza kuchapisha aina tisa (9) za vitabu ambazo ni sawa na nakala 30,000. Vitabu hivi vimesambazwa katika shule 146 zilizoko katika Programu ya Usomaji, maktaba za jamii, na nakala 300 maktaba zilizoko mikoani.
2.      Vitabu hivyo vimeongeza uwepo wa vitabu vya kujisomea shuleni katika lugha ya Kiingereza.
3.      Baadhi ya wachapishaji wameweza kuuza vitabu vyao katika nchi jirani za Afrika Mashariki.
4.      Tuzo hii imewezesha kutambua waandishi mahiri wa lugha ya Kiingereza.
5.      Tuzo hii inaunga mkono Mkukuta kwa kutoa mafunzo kwa wadau na kutoa zawadi nono kwa washindi.
6.      Kwa kupitia Tuzo hii waandishi wa Kitanzania wamehamasika kuandika miswada ambayo inahaririwa  na kuchapishwa kwa ubora wa hali ya juu.
7.      Warsha za waandishi zimewawezesha kujifunza mbinu za uandishi wa riwaya kwa Kiingereza.
8.      Serikali imeweza kuutambua Mradi na kumshukuru mfadhili wa Mradi, jambo linaonyesha heshima kwa mfadhili huyo.
9.        Aina 3 za vitabu chini ya Mradi vimeteuliwa kutumika kama vitabu vya fasihi ya kiingereza kwa madarasa ya kidato cha 3-4 na 5-6 kuanzia Julai 2012. Vitabu hivyo ni Face Under the Sea, The Best is Yet to Come na Tree Land the Land of Laughter.
Changamoto
-          Wachapishaji wengi wa vitabu wako katika miji mikubwa na hasa Dar es Salaam. Mikoani kuna wachapishaji wachache sana. Hali hii inawafanya waandishi chipukizi kutoka mikoani kushindwa kushiriki katika mashindano.
-          Waandishi wengi hawana mafunzo ya kutosha na mbinu mbali mbali za uandishi kuwawezesha kuandika miswada iliyo bora.
-          Tuzo hii inapata ugumu wa kuwafikia waandishi wengi zaidi hasa walio pembezoni mwa nchi.

Wito unatolewa kwa wachapishaji walioko mikoani kutafuta waandishi chipukizi na kuwasaidia ili waweze kushiriki.

CHANZO: Blogu ya Hakingowi  

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...