Kimya (Muyaka bin Haji)
"Kimya kina mshindo mkuu," || ndivyo wambavyo wavyele.
Kimya chataka k'umbuu, || viunoni mtatile:
Kimya chataka k'umbuu, || viunoni mtatile:
Kimya msikidharau, || nami sikidharawile.
Kimya
kina mambo mbele
Tahadharini na kimya.
Kimya ni kinga kizushi || kuzukia wale wale.
Kimya kitazua moshi || mato msiyafumbule.
Kimya kina mshawishi || kwa daima na milele.
Kimya kina
mambo mbele:
Tahadharini
na kimya.
Kimya vuani maozi || vuani mato muole!
Kimya kitangusha mwanzi || mwendako msijikule.
Kimya chatunda p'um'zi || kiumbizi kiumbile!
Kimya kina
mambo mbele:
Tahadharini
na kimya.
(Muyaka bin Haji, 1776-1840)
Comments
Napenda kumalizia ujumbe wangu huu kwa kukushukuru kwa kunisaidia kusambaza fikra zangu katika blogu ya wavuti.
Wahenga walituasa, kunyamaa ni dhahabu,
Tuuache ububusa, kila tunachojaribu,
Tujipgeni msasa, kabla ya kuhutubu,
Ukimya una darasa, kunyamaa ni dhahabu.
Watakuona galasa, wengine wakusulubu,
Ukitumia fursa, fikra ukaharibu,
Kaa kimya na kuasa, kuliko mambo haribu
Ukimya una darasa, kunyamaa ni dhahabu.