Sunday, September 11, 2016

Umuhimu wa Kusoma Vitabu

Kusoma vitabu kuna manufaa mengi kwa mtu binafsi na kwa jamii. Tunaweza kuitafakari kauli hii kwa namna nyingi. Binafsi, daima ninakumbuka usemi wa Ernest Hemingway, "There is no friend more loyal than a book," yaani hakuna rafiki wa kweli kuzidi kitabu. Ni kauli fupi na rahisi kukumbukwa, lakini ninaiona kuwa yenye ukweli kabisa.

Kitabu ni rafiki ambaye yuko kwa ajili yako muda wowote unapomhitaji. Kitabu kinaweza kuwa mshauri wako, kiongozi wako, nguzo ya kuitegemea.

Akili ya binadamu inahitaji matunzo, sawa na bustani. Bustani inahitaji kurutubishwa na kupaliliwa. Ikiachwa ivamiwe na magugu, inageuka kichaka. Kusoma vitabu ni kurutubisha akili na kuipalilia. Kama mtu anaweza, ni muhimu kusoma vitabu vya aina mbali mbali: vya siasa, saikolojia, fasihi, sayansi, maisha ya watu maarufu, falsafa, historia, uchumi, na kadhalika.

Ni makosa kudhani kuwa kusoma vitabu kunawahusu wanafunzi na waalimu pekee. Kila mtu anapaswa kusoma vitabu. Tutafakari manufaa yake kwa afya ya akili ya binadamu kama yalivyoelezwa kwa ufupi katika makala hii. 

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...