Thursday, November 11, 2021

Msomaji na Mpiga Debe Wangu Aikwaa Tuzo

Jana niliandika taarifa za msomaji na mpiga debe wangu Joy Zenz, mKenya aishiye uJerumani.

Napenda niseme kuwa juhudi zake za kuwaunganisha akina mama waAfrika waliko Ulaya na kwingineko na kuwahamasisha katika masuala ya maendeleo kwao na kwa bara la Afrika yamemfanya atambuliwe na kutuzwa kwa namna mbali mbali.

Leo nimeona taarifa kuwa ameikwaa tuzo muhimu ya Global Africa Awards. Nimefurahi na ninampongeza kwa dhati msomaji wangu huyu na mpiga debe.

1 comment:

Mbele said...

Hotuba yake ya kupkea tuzo hii hapa

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...