Saturday, November 6, 2021

Msomaji Wangu Mpya, mTanzania wa Czech

Wiki hii ya kwanza ya Novemba, 2021, nimemmpata msomaji mpya, Corona Cermak, mTanzania aishiye Jamhuri ya Czech. Nilisikia jina lake kwa mara ya kwanza kutoka kwa dada Joy Wanjiru Zenz, mKenya aishiye uJerumani, ambaye aliniambia kuwa kuna huyu mTanzania mwandishi aishiye Czech.

Katika kufuatilia Facebook, YouTube, na Instagram, nimeona shughuli za Corona, za ufundishaji wa kiSwahili na uandishi wa vitabu vya watoto. Vitabu alivyochapisha ni The Rooster's VoiceSauti ya Jogoo, na Grandma Pipi and the Roses.

Juzi nilimwandikia kuwa nimeagiza vitabu vyake Amazon, naye hima akaniletea picha akiwa ameshika kitabu changu, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. alichoagiza hivi karibuni mtandaoni.

Mara tu baada ya kukipata kitabu changu, amekisoma na kukiongelea mitandaoni Instagram na Facebook akiwahimiza watu waendao Marekani, Ulaya, na Tanzania wakisome. Amesema pia kuwa ameagiza kitabu changu cha Matengo Folktales. Ni bahati njema kufahamiana na mwalimu na mwandishi mwenzangu, mTanzania aishiye ughaibuni. Tunategemea kubadilishana mawazo na uzoefu.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...