Sunday, November 7, 2021

Simulizi za Wanawake waAfrika Waishio Ulaya


Ninaandika ujumbe huu nikiwa ninavisubiri vitabu viwili vya wanawake waAfrika waishio Ulaya. Napenda nielezee jinsi nilivyopata taarifa za vitabu hivi.

Tarehe 31 Mei hadi 4 Juni mwaka huu nilishiriki mkutano mkubwa mtandaoni, "Trade With Africa Business Summit." Mwandaaji, Toyin Umesiri, alikuwa ameniomba nikazungumzie kitebu changu kiitwacho Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Nilifanya hivyo, nikijikita katika kuongelea vipengele vya tamaduni vinavyohitaji kuzingatiwa katika biashara baina ya waAfrika na waMarekani.


Kwenye mkutano ule, nilipata kufahamiana na mtoa mada Joy Wanjiru Zenz, mama mKenya aishiye uJerumani na ni mwanzilishi na mwendeshaji wa jumuia ya wanawake waAfrika waishio Ulaya. Alishuhudia jinsi kitabu changu kilivyokuwa kinatajwa na baadhi ya washiriki wa mkutano.

Siku kadhaa baada ya mkutano, Joy nami tuliwasiliana,  akanieleza kuwa wanajumuia wake wamechapisha vitabu kuhusu maisha yao Ulaya. Nilivutiwa na taarifa hii. Ninayafahamu maisha ya waAfrika Marekani, lakini si Ulaya. Ilibidi nimwambie Joy kuwa ninahitaji vitabu hivi. Ninavisubiri kwa hamu.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...