Showing posts with label Notes on Okot p'Bitek's Song of Lawino. Show all posts
Showing posts with label Notes on Okot p'Bitek's Song of Lawino. Show all posts

Thursday, October 19, 2017

"Men Made Out of Words" ( Wallace Stevens)

Wallace Stevens ni mmoja wa washairi maarufu wa Marekani. Mara ya kwanza kupata fursa ya kuyasoma mashairi yake ni nilipokuwa ninasomea shahada ya uzamifu katika huo kikuu cha Wisconsin-Madison,1980-86. Nilichukua kozi kadhaa katika idara ya ki-Ingereza, mojawapo ikiwa "Poetry." Alitufundisha profesa John Brenkman.

Profesa Brenkman alikuwa na mtindo wa kufundisha ambao ulilifanya somo la "Poetry" livutie. Kwa uzoefu wangu wa kabla ya hapo, katika kusoma Tanzania, ushairi wa ki-Ingereza ndilo lilikuwa somo gumu kuliko mengine. Nilidokeza jambo hilo katika kijitabu changu cha Notes on Okot p Bitek's Song of Lawino.

Tangu nilipofundishwa na Profesa Brenkman, jina la Wallace Stevens limekuwa linanivutia, na daima niko tayari kusoma mashairi yake. Huu ni ushahidi wa jambo ambalo linafahamika vizuri, yaani namna mwalimu bora anavyoweza kumwathiri mwanafunzi. Jana nimeangalia kitabu changu cha mashairi, The Voice That is Great Within Us, na shairi moja lililonivutia ni "Men Made Out of Words," la Wallace Stevens. Ni shairi ambalo limeandikwa kwa uchache wa maneno na tamathali za usemi, na falsafa yake inachangamsha bongo.

MEN MADE OUT OF WORDS (Wallace Stevens)

What should we be without the sexual myth,
The human revery or poem of death?

Castratos of moon-mash--Life consists
Of propositions about life. The human

Revery is a solitude in which
We compose these propositions, torn by dreams,

By the terrible incantations of defeats
And by the fear that defeats and dreams are one.

The whole race is a poet that writes down
The eccentric propositions of its fate.


Wednesday, April 6, 2016

"Song of Lawino" Yatimiza Miaka 50

Mwaka huu, Song of Lawino, utungo maarufu wa Okot p'Bitek wa Uganda, unatimiza miaka hamsini tangu uchapishwe. Utungo huu, ambao unafahamika kama wimbo, ulichapishwa na East African Publishing House mwaka 1966 ukapata umaarufu tangu mwanzo.

Ulisomwa mashuleni na katika jamii kote Afrika Mashariki na sehemu zingine. Ulileta msisimko na upeo mpya katika dhana ya ushairi katika ki-Ingereza, na ulichochea washairi wengine kutunga kwa mtindo aliotumia Okot p'Bitek, ambao ulijaa athari za ushairi wa jadi wa ki-Afrika.

Siku chache zilizopita, niliandika katika blogu hii kuwa nimechapisha mwongozo wa Song of Lawino. Kitu ambacho sikusema ni kuwa nilikuwa na sababu ya kuchapisha mwongozo huu wakati huu, na sababu yenyewe ni hayo maadhimisho ya miaka 50.

Nilisoma taarifa, zaidi ya mwaka mmoja uliopita, kwamba idara ya "Literature" ya Chuo Kikuu cha Makerere ilikuwa inaandaa maadhimisho ya kumbukumbu hii, ambayo yangehusisha mihadhara na shughuli zingine. Ingekuwa niko Afrika Mashariki, ningeshiriki. Kwangu ingekuwa fursa sio tu ya kushiriki maadhimisho, bali pia kujikumbusha ziara ambazo niliwahi kufanya katika Chuo Kikuu cha Makerere.

Mara ya kwanza, mwaka 1978, nilienda kuhudhuria mkutano wa waalimu wa "Literature" kutoka vyuo vikuu vya Afrika Mashariki, na mara ya pili, mwaka 1990, nilikwenda kama mtahini wa nje katika idara ya "Literature and Mass Communications."

Kwa vile nilijua kuwa nisingeweza kuhudhuria maadhimisho, niliamua kuendelea kurekebisha mswada wa mwongozo wa Song of Lawino ambao nilikuwa nimeanza kuuandika miaka yapata ishirini iliyopita. Nilijiwekea lengo la kuchapisha mwongozo huu wakati huu wa maadhimisho ya miaka 50. Nafurahi kuwa nimefanikisha azma yangu.

Kwa mujibu wa taarifa nilizozisoma, maadhimisho yalifana. Ingawa shughuli rasmi zilifanyika katika Chuo Kikuu cha Makerere, taarifa za maadhimisho haya zilizagaa katika vyombo vya habari nchini Uganda. Mifano ni taarifa hii hapa na hii hapa.

Shughuli moja iliyonivutia katika maadhimisho haya ni kuzinduliwa kwa tafsiri ya Luganda ya Song of Lawino. Wanafasihi tunafahamu kuwa utungo huu una historia ndefu ya kutafsiriwa. Nimegusia suala hilo katika mwongozo wangu. Hadi leo, kuna tafsiri katika lugha zaidi ya thelathini. Kwa njia hii, umaarufu wake unaendelea kuenea ulimwenguni.


Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...