Showing posts with label ziwa nyasa. Show all posts
Showing posts with label ziwa nyasa. Show all posts

Friday, August 5, 2011

Mitaani Mbamba Bay

Agosti tarehe 2 nilisafiri kutoka kijijini kwangu Lituru nikapitia Mbinga, na kufika Mbamba Bay, mwambao wa Ziwa Nyasa kwa matembezi.

Mbamba Bay, ingawa mji mdogo sana, unavutia kwa utulivu wake na mazingira, ukiwa ufukweni mwa Ziwa linalomeremeta kwa maji yake maangavu, kama nilivyowahi kuandika hapa.

Nilikuwa na bahati kwamba tarehe 3 Agosti ilikuwa siku ya jua na hali ya hewa ya kuvutia sana. Nami nilitumia fursa hii vilivyo. Niliteremkia ufukweni kufurahia upepo mwanana na mandhari murua ya Ziwa.


Kukaa nje ya nchi yako kunakupa mtazamo tofauti wa masuala ya nchi yako. Kwa mfano, hapa Tanzania, watoto wetu wana uhuru sana wa kucheza na kuzunguka mitaani, tofauti na Marekani, ambako watoto huangaliwa sana muda wote na wazazi au walezi wao, kwani si salama kuwaacha watoto bila uangalizi. Wa-Marekani wanaokuja huku kwetu wanashangaa wanapowaona watoto wakijizungukia wenyewe mitaani, raha mstarehe. Nimeongelea tofauti hizo katika kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.

Joto la Mbambay ni kishawishi kikubwa cha kutafuta sehemu ya kujipatia kinywaji baridi. Nami nilisogea baa hii iitwayo Bush House, nikatuliza kiu.



Hali ya Mbamba Bay ni ya utulivu usio kifani. Ni mahali pazuri kwa mapumziko. Kadiri siku zinavyopita, nina imani kuwa Mbamba Bay patakuwa kivutio kikubwa kwa watalii wa nje na ndani ya nchi. Nami niliamua kufika Mbamba Bay ili kupiga picha nichangie katika kuitangaza sehemu hii ya Tanzania.










Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...