Siku chache zilizopita, niliweka makala kuhusu mrembo hapa katika blogu yangu. Lengo langu lilikuwa kuchochea mjadala kuhusu suala la urembo, ambalo, kama nilivyogusia, nimelijadili katika kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.
Nimeona picha nyingine ya warembo katika mtandao wa Facebook, ambayo naileta hapa. Sisi tuliokulia vijijini Afrika tunaweza kusema kuwa ingekuwa bora kama hao warembo wangejisitiri vizuri zaidi kimavazi. Lakini huenda hao si wa-Afrika. Hapa Marekani, kwa mfano, wakati wa joto, watu wengi huvaa vivazi ambavyo kwetu tunaviona si vya heshima, lakini hapa wanaona ni sawa.
Wednesday, May 30, 2012
Tuesday, May 29, 2012
Tamko la Askofu Mkuu Kufuatia Vurugu za Zanzibar
TAMKO LA ASKOFU MKUU WA TANZANIA ASSEMBLIES OF GOD, DK.BARNABAS
MTOKAMBALI, KUHUSU MATUKIO YANAYOASHIRIA UVUNJIFU WA AMANI NCHINI.
Kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na mfululizo wa matukio yanayoashiria
uvunjifu wa amani, umoja na utengamano wa taifa letu la Tanzania, haya
ndiyo yanayonisukuma kutoa tamko hili leo ili kuonya na kushauri.
Katika siku za karibu kiumeibuka makundi mbalimbali ya kidini ambayo
yalianza kutoa matamko yenye kuchochea ghasia za kidini Tanzania, na
pengine kauli hizo ndizo zinazotimizwa kwa vitendo hivi sasa.
Miongoni mwa matukio hayo ni:
Januari sita mwaka huu, kikundi kimoja kinachoitwa JUAKATA, kiliitisha
kongamano la kujadili katiba mpya Tanzania, kwa upande wa Waislam.
Katika kongamano hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee,
Dar es Salaam kauli zifuatazo:
1. Lazima Rais ajaye atoke Zanzibar
2. Kukabiliana na ukuaji wa kasi wa dini ya Kikristo
3. Kupinga Muungano ili kuupa nguvu Uislamu
4. Kupigana kufa na kupona kutetea maslahi yao wakati huu wa kuandaa
katiba mpya.
Kauli hizo zilitolewa na Sheikh Nasor Mohameed, kutoka Zanzibar,
ambaye alikuwa mgeni rasmi. Baadaye zikaandaliwa kanda za CD
zilizosambaza ujumbe huo.
Uchunguzi unaonesha kuwa miongoni mwa makanisa yaliyochomwa hivi
karibuni huko Zanzibar ni ya EAGT, Elimu Pentecost na TAG, Anglikana,
Katoliki na FPCT, hivyo kujenga taswira ya ubaguzi wa kidini ambao
kama hautapatiwa dawa unaweza kuligawa taifa la Tanzania kama
ilivyotokea Nigeria na kwingineko barani Afrika.
Hofu yangu ni kuwa, roho hii ya ubaguzi wa kidini ambayo Baba wa Taifa
hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliifananisha na dhambi ya kula
nyama ya mtu, imekuwa ikiyatafuna mataifa ya Afrika kama ifuatavyo:
1. Mwaka 2000, vuguvugu la kuanzishwa kwa utawala wa Kiislamu
(Sharia), lilianza kwenye majimbo ya Kaskazini mwa Nigeria, miaka
michache baadaye majimbo kadhaa yakajitangazia sheria hizo na tangu
wakati huo kumekuwa na mapambano yasiyoisha. Takwimu zinaonesha kuwa
katika miaka ya karibuni zaidi ya Wakristo 500 wameuawa kikatili na
makanisa kuchomwa moto.
2. Roho hii imekuwa ikienea kwa kasi katika maeneo mbali mbali ya
Afrika ambapo imelikumba taifa la Mali, majimbo ya kaskazini tayari
yametangaza kujitenga na kuna vuguvugu lenye kuhusisha mapigano ya
silaha.
3. Itakumbukwa kuwa wiki chache tu zilizopita vuguvugu hili la kudai
utawala wa kidini liliibuka nchini Kenya ambapo watu wanaojiita
wanaharakati walianzisha madai ya kutaka eneo la Pwani kujitenga na
Jamhuri ya Kenya na kujitangazia taifa la Kiislamu.
4. Ni wakati huu ambao kundi la Uamsho linalopinga kuandikwa kwa
katiba mpya kabla ya kuitishwa kwa kura ya maoni ili wanzazibar waamue
kuhusu Muungano liliibuka na kuanzisha ghasia Zanzibar ambazo
zimepelekea makanisa kadhaa kuchomwa moto na mali kuharibiwa, huku
watu wa bara wakitishiwa maisha.
USHAURI WANGU KWA SERIKALI NA VIONGOZI WA DINI
Ni wajibu wa kila Mtanzania kutii sheria na mamlaka kwa kuwa zimewekwa/
kuruhusiwa na Mungu, hivyo kuziasi ni Kumuasi Mungu, yaani ni dhambi.
Hivyo kila Mtanzania anastahili kukumbuka wajibu wake wa kutii
mamlaka.
Viongozi wenzangu wa dini wakumbuke kuwa wana wajibu mkubwa katika
jamii, na jamii inawasikiliza hivyo ni vyema wakawa makini katika
matamshi na maelekezo yao ili wasiwe chanzo cha kuchochea vurugu za
kidini na uvunjaji wa amani.
Ni vyema wakati huu wa kuandikwa kwa katiba mpya, kila kikundi
kikafuata utaratibu uliowekwa badala ya kuchochea ghasia ambazo
madhara yake yatawakumba watanzania wote ikiwa ni pamoja na wao
wenyewe watoto na wajukuu zao.
Pia ningependa kuwashauri viongozi wa serikali kusimama imara katika
kusimamia sheria na haki, na kuepuka kauli au vitendo vitakavyofanya
baadhi ya watanzania kudhani kuwa hawatendewi haki.
Ni vema ieleweke kuwa matukio kama haya ya uvunjaji wa amani
yasipodhibitiwa na kukomeshwa haraka yanaweza kuumba chuki ambayo
inaweza kuibua mlipuko mkubwa na machungu kwa wananchi na matokeo yake
yakawa mabaya kwa Taifa zima. Hekima na busara inatufundisha kuwa
tusipoziba ufa tutajenga ukuta.
Ni vyema wenye dhamana ya kuongoza wakakumbuka kuwa wanawajibu mbele
ya Mungu aliyewaweka au kuwaruhusu kuingia madarakani na siku moja
watatoa hesabu mbele zake.
Mwisho, natoa wito kwa watanzania wenzangu tuulinde umoja, amani na
utengamano wa taifa letu, tuikimbie dhambi ya ubaguzi kwa kuwa
tukiiruhusu itatuangamiza sote. Tuliombee taifa letu na kukiwa na
mbegu ya chuki tuimalize kwa njia ya majadiliano na vikao vya pamoja
vinavyohusisha viongozi wa dini zote na serikali pia.
Imetolewa leo 28/05/2012
Na Dk. Barnabas Mtokambali
Askofu Mkuu wa TAG
MTOKAMBALI, KUHUSU MATUKIO YANAYOASHIRIA UVUNJIFU WA AMANI NCHINI.
Kwa kipindi kirefu sasa kumekuwa na mfululizo wa matukio yanayoashiria
uvunjifu wa amani, umoja na utengamano wa taifa letu la Tanzania, haya
ndiyo yanayonisukuma kutoa tamko hili leo ili kuonya na kushauri.
Katika siku za karibu kiumeibuka makundi mbalimbali ya kidini ambayo
yalianza kutoa matamko yenye kuchochea ghasia za kidini Tanzania, na
pengine kauli hizo ndizo zinazotimizwa kwa vitendo hivi sasa.
Miongoni mwa matukio hayo ni:
Januari sita mwaka huu, kikundi kimoja kinachoitwa JUAKATA, kiliitisha
kongamano la kujadili katiba mpya Tanzania, kwa upande wa Waislam.
Katika kongamano hilo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee,
Dar es Salaam kauli zifuatazo:
1. Lazima Rais ajaye atoke Zanzibar
2. Kukabiliana na ukuaji wa kasi wa dini ya Kikristo
3. Kupinga Muungano ili kuupa nguvu Uislamu
4. Kupigana kufa na kupona kutetea maslahi yao wakati huu wa kuandaa
katiba mpya.
Kauli hizo zilitolewa na Sheikh Nasor Mohameed, kutoka Zanzibar,
ambaye alikuwa mgeni rasmi. Baadaye zikaandaliwa kanda za CD
zilizosambaza ujumbe huo.
Uchunguzi unaonesha kuwa miongoni mwa makanisa yaliyochomwa hivi
karibuni huko Zanzibar ni ya EAGT, Elimu Pentecost na TAG, Anglikana,
Katoliki na FPCT, hivyo kujenga taswira ya ubaguzi wa kidini ambao
kama hautapatiwa dawa unaweza kuligawa taifa la Tanzania kama
ilivyotokea Nigeria na kwingineko barani Afrika.
Hofu yangu ni kuwa, roho hii ya ubaguzi wa kidini ambayo Baba wa Taifa
hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliifananisha na dhambi ya kula
nyama ya mtu, imekuwa ikiyatafuna mataifa ya Afrika kama ifuatavyo:
1. Mwaka 2000, vuguvugu la kuanzishwa kwa utawala wa Kiislamu
(Sharia), lilianza kwenye majimbo ya Kaskazini mwa Nigeria, miaka
michache baadaye majimbo kadhaa yakajitangazia sheria hizo na tangu
wakati huo kumekuwa na mapambano yasiyoisha. Takwimu zinaonesha kuwa
katika miaka ya karibuni zaidi ya Wakristo 500 wameuawa kikatili na
makanisa kuchomwa moto.
2. Roho hii imekuwa ikienea kwa kasi katika maeneo mbali mbali ya
Afrika ambapo imelikumba taifa la Mali, majimbo ya kaskazini tayari
yametangaza kujitenga na kuna vuguvugu lenye kuhusisha mapigano ya
silaha.
3. Itakumbukwa kuwa wiki chache tu zilizopita vuguvugu hili la kudai
utawala wa kidini liliibuka nchini Kenya ambapo watu wanaojiita
wanaharakati walianzisha madai ya kutaka eneo la Pwani kujitenga na
Jamhuri ya Kenya na kujitangazia taifa la Kiislamu.
4. Ni wakati huu ambao kundi la Uamsho linalopinga kuandikwa kwa
katiba mpya kabla ya kuitishwa kwa kura ya maoni ili wanzazibar waamue
kuhusu Muungano liliibuka na kuanzisha ghasia Zanzibar ambazo
zimepelekea makanisa kadhaa kuchomwa moto na mali kuharibiwa, huku
watu wa bara wakitishiwa maisha.
USHAURI WANGU KWA SERIKALI NA VIONGOZI WA DINI
Ni wajibu wa kila Mtanzania kutii sheria na mamlaka kwa kuwa zimewekwa/
kuruhusiwa na Mungu, hivyo kuziasi ni Kumuasi Mungu, yaani ni dhambi.
Hivyo kila Mtanzania anastahili kukumbuka wajibu wake wa kutii
mamlaka.
Viongozi wenzangu wa dini wakumbuke kuwa wana wajibu mkubwa katika
jamii, na jamii inawasikiliza hivyo ni vyema wakawa makini katika
matamshi na maelekezo yao ili wasiwe chanzo cha kuchochea vurugu za
kidini na uvunjaji wa amani.
Ni vyema wakati huu wa kuandikwa kwa katiba mpya, kila kikundi
kikafuata utaratibu uliowekwa badala ya kuchochea ghasia ambazo
madhara yake yatawakumba watanzania wote ikiwa ni pamoja na wao
wenyewe watoto na wajukuu zao.
Pia ningependa kuwashauri viongozi wa serikali kusimama imara katika
kusimamia sheria na haki, na kuepuka kauli au vitendo vitakavyofanya
baadhi ya watanzania kudhani kuwa hawatendewi haki.
Ni vema ieleweke kuwa matukio kama haya ya uvunjaji wa amani
yasipodhibitiwa na kukomeshwa haraka yanaweza kuumba chuki ambayo
inaweza kuibua mlipuko mkubwa na machungu kwa wananchi na matokeo yake
yakawa mabaya kwa Taifa zima. Hekima na busara inatufundisha kuwa
tusipoziba ufa tutajenga ukuta.
Ni vyema wenye dhamana ya kuongoza wakakumbuka kuwa wanawajibu mbele
ya Mungu aliyewaweka au kuwaruhusu kuingia madarakani na siku moja
watatoa hesabu mbele zake.
Mwisho, natoa wito kwa watanzania wenzangu tuulinde umoja, amani na
utengamano wa taifa letu, tuikimbie dhambi ya ubaguzi kwa kuwa
tukiiruhusu itatuangamiza sote. Tuliombee taifa letu na kukiwa na
mbegu ya chuki tuimalize kwa njia ya majadiliano na vikao vya pamoja
vinavyohusisha viongozi wa dini zote na serikali pia.
Imetolewa leo 28/05/2012
Na Dk. Barnabas Mtokambali
Askofu Mkuu wa TAG

Monday, May 28, 2012
Uamsho (Zanzibar): Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Jumuia ya Uamsho (Zanzibar) imetoa taarifa kufuatia maandamano na kisha vurugu zilizotokea Zanzibar wiki hii. Nimezipata picha na taarifa kutoka Zanzibar Yetu. Inatia moyo kuona jinsi taarifa hiyo inavyoanza kwa kumtaja Allah na Mtume Muhammad na kisha kusisitiza suala la amani na kuheshimu haki za watu wote. Inatia moyo kuona jinsi taarifa hii inavyotaja wazi kuwa tunawajibika kuheshimiana, kutunza amani, kuheshimu mali na haki za kila mtu, ikiwemo kuheshimu dini na nyumba za ibada. Hayo ni mawaidha mema kabisa.
Ingekuwa mawaidha hayo yanatolewa na kusisitizwa kila wakati, katika mihadhara yote na mahubiri mengine, nje na ndani ya nyumba za ibada, nina imani amani ingedumu katika jamii. Lakini je, mawaidha hayo ndiyo yanayotolewa na kusisitizwa katika mihadhara na mahubiri yote?
Hapa kushoto ni picha mojawapo ya uharibifu uliofanyika wakati wa vurugu za wiki hii, ambapo kanisa lilichomwa moto, sambamba na hilo gari.
Waumini wa dini zote tunaweza kunukuu misahafu na kuthibitisha kuwa dini zetu zinafundisha amani. Lakini jambo la msingi zaidi sio kunukuu na kujadili misahafu, bali matendo yetu katika jamii na mbele ya Muumba. Hiki ndicho kigezo muhimu zaidi cha kupima kama sisi ni waumini kweli.
Taarifa tulizopata katika vyombo vya habari zimesema kuwa maandamano haya ya Uamsho yalikuwa ya kupinga Muungano. Tulisoma pia kuwa wana-Uamsho wanataka kupeleka malalamiko yao Umoja wa Mataifa.
Kilichonishangaza ni jinsi wana-Uamsho walivyojifanya kuwa wao ndio sauti ya wa-Zanzibari. Wanachotaka wao kifanyike. Nashangaa kwa nini wana-Uamsho wawe na msimamo huo, wakati wao ni sehemu tu ya jamii ya Zanzibar na kuna wenzao wenye mitazamo tofauti. Kwa mfano, Sheikh Muhidin Zubeir Muhidin, katibu wa jumuia ya maimam wa Zanzibar (JUMAZA) amenukuliwa kwamba "alisema Jumuiya yake ni tofauti na Jumuiya ya Uamsho hivyo watu wasizichanganye." Soma hapa.
Kwa nini wana-Uamsho wawe na msimamo wao huu hasa wakati huu ambapo wa-Tanzania tuko katika mchakato wa kutafuta maoni kuhusu Katiba na tume imeshaundwa ambayo itasikiliza maoni hayo. Nini kinachowafanya wana-Uamsho wachukue hatua ya kutaka kwenda Umoja wa Mataifa, wakati kuna hiyo fursa ya kuelezea mtazamo wao na kujumuika na wa-Tanzania wengine katika kutafuta suluhu ya matatizo? Kuhusu nani aliyechoma moto kanisa na kufanya uharibifu mwingine, tutajua baada ya uchunguzi kukamilika, na bora zaidi iwapo kesi itafika mahakamani na kuamuliwa.
Baada ya hizo kauli zangu, naleta tamko la Jumuia ya Uamsho:
THE ASSOCIATION FOR ISLAMIC MOBILISATION AND PROPAGATION
P. O. BOX: 1266
Tel: +255-777-419473 / 434145-
FAX +255-024-2250022
E-Mail: jumiki@hotmail.com
MKUNAZINI ZANZIBAR
Tarehe 27MAY2012
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kila sifa njema anastahiki ALLAH (S.W) na Rehma na Amani zimuendee
Mtume Muhammad (S.A.W), ahli zake, Maswahaba zake na walio wema katika
Uislamu.
Jumuia ya UAMSHO inatoa taarifa rasmi kwa umma wa Wazanzibari na
Watanzania wote kwa ujumla kwamba haihusiki na vitendo vyote vya
uvunjaji wa amani vilivyotokea usiku wa tarehe 26 Mei 2012. Kama
alivyosema Mtume (S.A.W) katika Hijatul Wadaa, kwamba ni haramu
kumwaga damu zenu, kuharibiana mali zenu, kuvunjiana heshma zenu ila
kwa haki ya Uislamu (maana yake pale mtu anapofanya kosa na
likathibitika atahukumiwa kwa hukmu ya Kiislamu). Vile vile Uislamu
unaheshimu nyumba za ibada (Makanisa, Mahekalu na n.k) zisivunjwe wala
zisiharibiwe.
Jumuia inatoa wito kwa Waislamu na Wazanzibari wote kuendelea
kudumisha amani na utulivu wa nchi na kutoharibu mali za serikali,
mali za wananchi, mali za taasisi za dini zenye imani tofauti, kwani
kufanya hivyo ni kwenda kinyume na mafundisho ya dini ya Kiislamu.
Jumuiya inayachukulia matukio yaliyotokea usiku wa jana, na
yanayoendelea tangu alfajiri leo, kama ni njama za makusudi za wale
wasioipendelea amani nchi hii, pamoja na kutaka kuipaka matope jumuiya
na kutaka kuzuia lengo la Wazanzibari kudai nchi yao.
Tunatoa wito kwa Jeshi la Polisi na Vyombo vyote vya Dola wafanye kazi
zao kama wanavyotakiwa kwa mujibu wa muongozo wa haki za binadamu kwa
Polisi na vikosi vingine unaosema kwamba polisi na vyombo vingine vya
dola wana jukumu la kutunza amani na utulivu na jukumu la kutoingilia
haki za watu. Kila mtu anayo haki ya kuwekewa mazingira muafaka ya
kitaifa na kimataifa yatakayomuwezesha kupata haki zake za binadamu.
Polisi na vyombo vingine vya dola wana jukumu la kutunza amani na
utulivu na jukumu la kutoingilia haki za watu isipokuwa tu kwa minajil
ya kulinda haki za wengine.
Polisi na vyombo vingine vya dola wana jukumu la kuheshimu, kulinda na
kutetea haki za binadamu kwa watu wote.
WABILLLAH TAWFIQ
Ingekuwa mawaidha hayo yanatolewa na kusisitizwa kila wakati, katika mihadhara yote na mahubiri mengine, nje na ndani ya nyumba za ibada, nina imani amani ingedumu katika jamii. Lakini je, mawaidha hayo ndiyo yanayotolewa na kusisitizwa katika mihadhara na mahubiri yote?
Hapa kushoto ni picha mojawapo ya uharibifu uliofanyika wakati wa vurugu za wiki hii, ambapo kanisa lilichomwa moto, sambamba na hilo gari.
Waumini wa dini zote tunaweza kunukuu misahafu na kuthibitisha kuwa dini zetu zinafundisha amani. Lakini jambo la msingi zaidi sio kunukuu na kujadili misahafu, bali matendo yetu katika jamii na mbele ya Muumba. Hiki ndicho kigezo muhimu zaidi cha kupima kama sisi ni waumini kweli.
Taarifa tulizopata katika vyombo vya habari zimesema kuwa maandamano haya ya Uamsho yalikuwa ya kupinga Muungano. Tulisoma pia kuwa wana-Uamsho wanataka kupeleka malalamiko yao Umoja wa Mataifa.
Kilichonishangaza ni jinsi wana-Uamsho walivyojifanya kuwa wao ndio sauti ya wa-Zanzibari. Wanachotaka wao kifanyike. Nashangaa kwa nini wana-Uamsho wawe na msimamo huo, wakati wao ni sehemu tu ya jamii ya Zanzibar na kuna wenzao wenye mitazamo tofauti. Kwa mfano, Sheikh Muhidin Zubeir Muhidin, katibu wa jumuia ya maimam wa Zanzibar (JUMAZA) amenukuliwa kwamba "alisema Jumuiya yake ni tofauti na Jumuiya ya Uamsho hivyo watu wasizichanganye." Soma hapa.
Kwa nini wana-Uamsho wawe na msimamo wao huu hasa wakati huu ambapo wa-Tanzania tuko katika mchakato wa kutafuta maoni kuhusu Katiba na tume imeshaundwa ambayo itasikiliza maoni hayo. Nini kinachowafanya wana-Uamsho wachukue hatua ya kutaka kwenda Umoja wa Mataifa, wakati kuna hiyo fursa ya kuelezea mtazamo wao na kujumuika na wa-Tanzania wengine katika kutafuta suluhu ya matatizo? Kuhusu nani aliyechoma moto kanisa na kufanya uharibifu mwingine, tutajua baada ya uchunguzi kukamilika, na bora zaidi iwapo kesi itafika mahakamani na kuamuliwa.
Baada ya hizo kauli zangu, naleta tamko la Jumuia ya Uamsho:
P. O. BOX: 1266
Tel: +255-777-419473 / 434145-
FAX +255-024-2250022
E-Mail: jumiki@hotmail.com
MKUNAZINI ZANZIBAR
Tarehe 27MAY2012
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kila sifa njema anastahiki ALLAH (S.W) na Rehma na Amani zimuendee
Mtume Muhammad (S.A.W), ahli zake, Maswahaba zake na walio wema katika
Uislamu.
Jumuia ya UAMSHO inatoa taarifa rasmi kwa umma wa Wazanzibari na
Watanzania wote kwa ujumla kwamba haihusiki na vitendo vyote vya
uvunjaji wa amani vilivyotokea usiku wa tarehe 26 Mei 2012. Kama
alivyosema Mtume (S.A.W) katika Hijatul Wadaa, kwamba ni haramu
kumwaga damu zenu, kuharibiana mali zenu, kuvunjiana heshma zenu ila
kwa haki ya Uislamu (maana yake pale mtu anapofanya kosa na
likathibitika atahukumiwa kwa hukmu ya Kiislamu). Vile vile Uislamu
unaheshimu nyumba za ibada (Makanisa, Mahekalu na n.k) zisivunjwe wala
zisiharibiwe.
Jumuia inatoa wito kwa Waislamu na Wazanzibari wote kuendelea
kudumisha amani na utulivu wa nchi na kutoharibu mali za serikali,
mali za wananchi, mali za taasisi za dini zenye imani tofauti, kwani
kufanya hivyo ni kwenda kinyume na mafundisho ya dini ya Kiislamu.
Jumuiya inayachukulia matukio yaliyotokea usiku wa jana, na
yanayoendelea tangu alfajiri leo, kama ni njama za makusudi za wale
wasioipendelea amani nchi hii, pamoja na kutaka kuipaka matope jumuiya
na kutaka kuzuia lengo la Wazanzibari kudai nchi yao.
Tunatoa wito kwa Jeshi la Polisi na Vyombo vyote vya Dola wafanye kazi
zao kama wanavyotakiwa kwa mujibu wa muongozo wa haki za binadamu kwa
Polisi na vikosi vingine unaosema kwamba polisi na vyombo vingine vya
dola wana jukumu la kutunza amani na utulivu na jukumu la kutoingilia
haki za watu. Kila mtu anayo haki ya kuwekewa mazingira muafaka ya
kitaifa na kimataifa yatakayomuwezesha kupata haki zake za binadamu.
Polisi na vyombo vingine vya dola wana jukumu la kutunza amani na
utulivu na jukumu la kutoingilia haki za watu isipokuwa tu kwa minajil
ya kulinda haki za wengine.
Polisi na vyombo vingine vya dola wana jukumu la kuheshimu, kulinda na
kutetea haki za binadamu kwa watu wote.
WABILLLAH TAWFIQ
Saturday, May 26, 2012
Wa-Tanzania Katika Shughuli za Kila Siku
Ninawawazia watu ninaowaona mitaani, kila mtu akiwa na harakati zake, mategemeo yake, na bila shaka wasi wasi na shida pia. Laiti ingewezekana kuongea na kila mtu na kuzipata habari zake.
Hapa ni Ubungo. Nilipiga picha hii nikiwa ndani ya basi kutokea mikoani. Nilivutiwa na huyu kijana mwenye mkokoteni, akiwa katika kujitafutia riziki. Barabara inavyopinda kushoto inaelekea Chuo Kikuu na Mwenge.
Hapa ni mjini Moshi.
Hapa ni kituo cha mabasi cha Msamvu, Morogoro.
Hapa ni Lyulilo, karibu na Matema Beach, Ziwa Nyasa. Ni siku ya soko, kama nilivyoelezea hapa.
Hapa ni Ubungo. Nilipiga picha hii nikiwa ndani ya basi kutokea mikoani. Nilivutiwa na huyu kijana mwenye mkokoteni, akiwa katika kujitafutia riziki. Barabara inavyopinda kushoto inaelekea Chuo Kikuu na Mwenge.
Hapa ni mjini Moshi.
Hapa ni kituo cha mabasi cha Msamvu, Morogoro.
Hapa ni Lyulilo, karibu na Matema Beach, Ziwa Nyasa. Ni siku ya soko, kama nilivyoelezea hapa.
Thursday, May 24, 2012
Tuesday, May 22, 2012
Makaa Yetu ya Mawe Yanakwenda Wapi?
Hapa ni Bandari ya Ndumbi iliyopo mwambao mwa ziwa Nyasa.Bandari hii inatumika kusafirishia makaa ya mawe ambayo yanachimbwa katika kijiji cha Ngaka wilayani Mbinga mkoani Ruvuma.Takwimu zinaonesha kuwa kila wiki zaidi ya tani 600 za makaa ya makaa ya mawe zinasafirishwa kupitia bandari hii kupelekwa sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi.Hata hivyo hakuna anayefahamu ukweli kuhusu kile ambacho kinasafirishwa kupitia bandari hiyo ambayo haina ofisi muhimu za serikali.
(Picha na maelezo na Albano Midelo, Maendeleo ni Vita)
(Picha na maelezo na Albano Midelo, Maendeleo ni Vita)
Mnadani Karatu
Tanzania ni nchi kubwa, yenye mengi ya kuvutia. Mwaka 2008, kwa mfano, nilishuhudia mnada katika mji wa Karatu. Watu walijaa hapo kwenye viwanja vya mnada. Walikuwepo wauzaji na wateja wa bidhaa na huduma mbali mbali. Wengine, kama mimi, tulienda kuangalia. Kulikuwa na mengi ya kuyaona na hata kustaajabia.
Siku ya mnada ni siku muhimu katika maisha ya watu wa sehemu hizo. Nami nikiwa maeneo hayo, sitakosa kuhudhuria.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...
-
Ukizunguka mitaani Dar es Salaam, utakuta matangazo mengi ya waganga wa kienyeji. Waganga hao wanatoka sehemu mbali mbali, kama vile Sumbaw...
-
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...
-
Leo napenda kukitambulisha kwako mdau kitabu muhimu cha ki-Swahili, Tenzi Tatu za Kale . Nilinunua nakala yangu miaka kadhaa iliyopita katik...





.jpg)
