Tuesday, November 15, 2011

Mhadhara Katika Chuo cha Mazingira, Minnesota

Leo nilikwenda Apple Valley, kuongea na wanafunzi wa Chuo cha Msomo ya Mazingira. Nilialikwa na mwalimu Todd Carlson, na wanafunzi wake hao wamekuwa wakishughulika na mada ya falsafa za jadi.

Kwa miaka mingi, mwalimu Carlson amekuwa akinialika kuongea na wanafunzi hao.





Katika kuwaandaa, Mwalimu Carlson anawapa sehemu kadhaa za kitabu cha Matengo Folktales wasome. Kutokana na maandalizi hayo, wanafunzi hao wanakuwa na duku duku na masuali mengi ya kuniuliza. Ni wanafunzi makini sana. Wanaulizia kuhusu utafiti wa fasihi simulizi na changamoto za uandishi masimulizi hayo, tafsiri, maana, falsafa na kadhalika, wakizingatia yale niliyoandika katika Matengo Folktales.

Kila ninapotembelea Chuo hiki, nawasimulia hadithi angalau moja kutoka katika Matengo Folktales. Leo niliwasimulia hadithi ya "Jitu Katika Shamba la Mpunga," ambayo ni chemsha bongo ya aina yake, tukatumia muda kuiongelea.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...