Saturday, July 21, 2012

Ziara ya Peramiho

Jana nilienda Peramiho, mji ulio karibu na Songea. kwa kweli, Peramiho haifahamiki kama mji. Ni misheni kubwa ya Kanisa Katoliki. Kuna kanisa kubwa, seminari kuu, hospitali, duka la vitabu, na kiwanda cha uchapishaji.

Nimefurahi kuona sehemu kadhaa za Peramiho.Picha nilizopiga nitaziweka katika blogu hii hivi punde, Insh'Allah.

Vile vile, nimepata fursa ya kutembelea chuo kikuu cha Songea, kinachoendeshwa na Kanisa Katoliki. Taarifa nitazileta hivi punde, Insh'Allah.

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

Usichelewe kuleta hizo habari na hizo picha nina usongo kweli wa kuona...

Mbele said...

Hatimaye, wiki nyingi baadaye, nimeanza kuzileta hizo picha, kama ulivyoziona hapa

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...