Wednesday, June 22, 2016

Mhadhiri wa Algeria Akifurahia Kitabu

Jana, katika ukurasa wangu wa Facebook, mhadhiri wa fasihi ya ki-Afrika katika chuo kikuu kimoja cha Algeria ameandika ujumbe kuhusu mchango wangu katika fasihi na elimu, akataja kijitabu changu, Notes on Achebe's Things Fall Apart. Hatufahamiani, isipokuwa katika Facebook.

Yeye ni mfuatiliaji wa kazi zangu za kitaaluma, na niliwahi kumpelekea nakala ya Notes on Achebe's Things Fall Apart. Ameandika:

Dear professor Joseph you're one of God's gifts to the world of literature and education. I always keep praying for you when I read you book Notes On Achebe's TFA. I love you so much dear. Greetings from Algeria.

Kwangu ujumbe huu ni faraja, hasa kwa kuwa unatoka kwa mhadhiri wa somo ambalo ndilo nililoandikia mwongozo. Ninafurahi kuwa mawazo yangu yanawanufaisha watu Algeria. Kijitabu hiki niliwahi kukiongelea katika blogu hii, nikataja kilivyoteuliwa kama mwongozo kwa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Cornell.

Taarifa za aina hii hazinifanyi nitulie na kujipongeza, bali napata motisha ya kuendelea kusoma, kutafakari, na kuandika. Kuandika miongozo ya kazi ya fasihi ni jukumu ambalo nimeendelea kulitekeleza, kama nilivyoandika katika blogu hii.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...