Saturday, April 21, 2018

Mdau Amechagua Kitabu

Jana nimeona taarifa iliyonigusa kwa namna ya pekee. Mdau ameweka mtandaoni picha inayoonekana kushoto, akiwa ameambatanisha ujumbe: "Decided to bring some required reading with me." yaani anasema ameamua kubeba vitabu muhimu vya kujisomea. Hakusema kama anasafiri, lakini ujumbe wake unaashiria hivyo.

Niliguswa kuona kitabu changu Africans and Americans: Embracing Cultural Differences ni kimojawapo alichochagua, nikaandika "I am humbled that you have my "Africans and Americans" book on your list," yaani "nimeishiwa nguvu kuona kuwa umetaja kitabu changu katika orodha yako." Jibu aliloandika ni "Yes! I'm learning a lot. It's funny too. Thanks for the enlightenment," yaani "Ndio! Ninajifunza mengi. Kitabu kinachekesha pia. Asante kwa uelimishaji."

Nimeguswa kwa namna ya pekee kwa sababu mdau huyu, ambaye anaonekana nami pichani hapa kushoto, ni mtu mwenye ushawishi katika jamii, kama nilivyowahi kuelezea katika blogu hii. Ninafarijika kuwa kitabu changu ambacho nilikichapisha mwaka 2005 bado kinafanikisha malengo niliyokuwa nayo wakati nilipokuwa ninakiandaa na kukiandika. Lengo kuu lilikuwa ni kuwaelimisha watu, hasa wa-Afrika na wa-Marekani, kuhusu tofauti za tamaduni zao, iwe ni kinga ya kuzuia migongano na kutoelewana. Ila, kama huyu mdau anavyosema, kitabu hiki, pamoja na kuwa kinaelimisha, ni burudani pia.

Ninaweka taarifa hii hapa katika blogu yangu, kwa sababu hapa ni mahali ninapotunzia kumbukumbu zangu, kama nilivyowahi kuelezea.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...