Showing posts with label kitabu cha Africans and Americans. Show all posts
Showing posts with label kitabu cha Africans and Americans. Show all posts

Sunday, June 12, 2011

Anonymous Anasema Kitabu Hiki Hakina Jipya

Kwa wasomaji wa blogu yangu hii na ile ya ki-Ingereza, habari za kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences sio ngeni. Wengi wamekisoma kitabu hiki na wengine wamechangia maoni yao katika blogu hizi na zingine.

Juzi ametokea anonymous kwenye blogu hii akaandika hivi: "Nimekisoma hakina chochote kipya, ni kama vitabu vingine."

Mimi kama mtafiti na mwalimu huhamasisha elimu na kuelimishana. Nilimpa ukumbi anonymous atuelimishe zaidi na pia kututajia hivyo vitabu vingine. Habari kamili iko kwenye sehemu ya maoni hapa. Hadi sasa anonymous hajasema kitu tena. Bado nasubiri.

Tuesday, June 7, 2011

Mwaliko Nyumbani kwa Wateja Wangu

Jana jioni nilikuwa nyumbani kwa familia inayoonekana katika hii picha. Ni familia ya Shannon Gibney, mwandishi chipukizi ambaye tayari ni maarufu.

Miaka michache iliyopita, Shannon Gibney alisoma kitabu changu cha Africans and Americans, akaandika mapitio katika Minnesota Spokesman Recorder, kama nilivyosema hapa.

Siku chache zilizopita alinialika nyumbani kwake kwa chakula cha jioni, tukapanga hiyo tarehe ya jana. Aliniambia kuwa mume wake, ambaye anatoka Liberia, na bado ni mgeni hapa Marekani, amekuwa akisoma kitabu changu.

Nilifurahi kukutana na familia hii. Kwa zaidi ya saa mbili nilizokuwa nao, maongezi yetu yalihusu masuala niliyoongelea katika kitabu, yaani tofauti za tamaduni za wa-Marekani na wa-Afrika. Wote wawili wanakifahamu vizuri sana kitabu hiki, na walikuwa wananikumbusha mengi, ingawa mimi ndiye mwandishi.

Huyu bwana aliezea mshangao wake kwa jinsi maelezo ya kitabu hiki yanavyofanana na hali ya Liberia, ingawa mimi mwandishi sijafika kule. Niliguswa na furaha yake kwamba niliyoandika yamemwelewesha mambo ya wa-Marekani ambayo yalikuwa yanamtatiza. Nami nashukuru kwa hilo.

Familia hii ilinikarimu vizuri sana, nami nimebaki nashangaa kwa jinsi uandishi wa kitabu unavyoweza kukujengea urafiki na watu kiasi hicho.

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...