Tuesday, February 8, 2011

Blogu Imenisaidia Darasani

Leo wakati muhula mpya unaanza hapa Chuoni St. Olaf, nimekutana na wanafunzi nitakaowafundisha somo la kuandika kwa ki-Ingereza. Kama kawaida, siku ya kwanza huwa ni ya kujitambulisha, kuelezea habari za somo, maana yake, falsafa na maadili yangu kama mwalimu, maana na mikakati ninayotumia katika kufundisha.

Katika kujitambulisha, huwa nawaeleza wanafunzi kuhusu nyumbani kwangu, shule nilizosoma, na nilivyoingia katika kazi ya ualimu, na imani yangu kuwa Mungu alitaka niwe mwalimu.

Leo wakati naanza kuelezea habari za nyumbani kwangu, nilikumbuka kuwa nilishaandika kwenye blogu. Basi, niliwasha kompyuta iliyomo darasani nikafungua blogu na wao wenyewe wakasoma kwenye skrini kubwa habari za Litembo.

Blogu imenisaidia kufikisha ujumbe wangu kwa ufanisi, kwani mbali ya maelezo kuna picha. Picha zinajieleza vizuri kuliko pengine hata maneno, jambo linalosisitizwa katika ule usemi kuwa picha ni sawa na maneno elfu. Niliwaambia kuwa nina picha nyingi za nyumbani kwangu na Tanzania kwa ujumla. Ni wazi kuwa ninazo fursa tele za kuendelea kuwajulisha walimwengu habari za kwetu.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...