TAMKO LA CCM MKOA WA MOROGORO KUHUSU VURUGU ZILIZOTOKEA RUAHA JANA JIONI

Ndugu
 wananchi Tarehe 24/4/2013 ulifanyika uchaguzi wa mwenyekiti wa Serikali
 ya kijiji cha Ruaha. Vyama vilivyoweka wagombea vilikuwa CCM na 
CHADEMA. Hata hivyo mgombea wa Chadema alienguliwa baada ya CCM 
kumuewekea pingamizi kwa sababu alikuwa na mapungufu yaliyomwondolea 
sifa ya kuwa mgombea kwa mujibu wa sheria. Hivyo basi CCM ilitangazwa 
mshindi na siku hiyo hiyo Chadema wakashinda kitongoji. 
Wana
 CCM waliyapokea matokea bila vurugu na wakakubali kuwa Mwenyekiti wa 
Kitongoji ni wa CHADEMA. Tarehe 09.05.2013 ili kuwa siku ya kukabidhiwa 
rasmi ofisi kwa Mwenyekiti mpya wa Kijiji cha Ruaha, lakini wenzetu 
CHADEMA wakataa kumkubali huyo Mwenyekiti na wakaamua kuanzisha vurugu 
kubwa sana katika kijiji cha Ruaha na maeneo ya karibu yaliosababisha 
uharibifu mkubwa wa mali.Wamechoma nyumba, wamefunga barabara na 
kusababisha uvunjifu mkubwa wa amnai eneo hilo. 
Tunalaani
 sana vurugu hizo zilizosababishwa na kundi la watu wenye nia mbaya na 
nchi hii wanaotaka kuivunja amnai tulionayo, wananchi wa morogoro na 
Watanzania kwa ujumla Tunavitaka vyombo vya ulinzi na usalama kuchukua 
hatua mara moja kurudisha amani ili wananchi waendelee na shuguli zao za
 kila siku za kujiletea maendeleo. Kwa wale wote waliochochea vurugu 
hizo wachukuliwe hatua mara moja na sheria ichukue mkondo wake.
Imetolewa CCM Morogoro
10.05.2012
 
 
 
 
No comments:
Post a Comment