Wednesday, May 8, 2013

Nukta Tano za Mwigulu Nchemba

Kwenye ukurasa wake wa Facebook, Ndugu Mohamedi Mtoi ameandika ujumbe ufuatao kuhusu mambo ya Mwigulu Nchemba, mbunge wa Iramba Magharibi kwa tiketi ya CCM:
---------------------------------------------------------------

NUKTA TANO (5) ZA MWIGULU KUKOSA HOFU YA MUNGU NA KUJAWA MAWAZO YA USHETANI NDANI YAKE.

Baada kufutwa kwa mashtaka ya ugaidi dhidi ya Rwekatare nimejiridhisha kuwa. Mwigulu hana utu, binadamu unapo kosa utu juu ya binadamu mwenzako unadondokea kwenye sifa za mnyama, lakini ukikubali kuwa wapo wanyama lakini pamoja na unyama wao wana tunu ya kumsaidia binadamu kwenye mambo mbalimbali kama vile kulima, kuwinda na hata kama kitoweo wakati wa maakuli. Basi mtu akikosa sifa za unyama (Mnyama) moja kwa moja anajivisha sifa za ushetani.

Kama hivyo ndivyo, leo Mwigulu Nchemba amedondokea kwenye sifa za ushetani! Sija muweka kwenye kundi hilo kwa bahati mbaya bali kwa matendo yenye hoja na tafakuri jadidi.

Kwa nini.

1. Kwa mipango yake ya
kishetani ya ugaidi kwa ajili unafuu na ujiko wa kisiasa, amesababisha Rwekatare
kuteseka mbaroni kwa takribani mwezi mmoja sasa. Mtu anaye
weza kutesa nafsi ya mtu mwingine hana tofauti na shetani anaye tesa roho na nyama za mwili wa binadamu.

2. Kwa mipango yake ya
kishetani, Mwigulu alishindwa kufikiria maradhi ya Rwekatare (Kisukari) maradhi
yanayo hitaji namna ya uangalizi maalumu kwenye vyakula na
hata mazoezi. Ni shetani pekee ndio mwenye
sifa ya kutomjali binadamu anaye teseka kwa maradhi. Hii ni zaidi ya sifa ya unyama maana mbwa au paka wako nyumbani anaweza kukuonea huruma.

3. Familia ya Rwekatare na hasa watoto wameteseka na
kuathirika kisaikolojia kwa kipindi chote ambacho baba yao alitegewa
mtego wa kishetani. Huenda huko mashuleni wameitwa "Watoto wa gaidi" Nani mwenye uwezo wa kupangusa maumivu ya kisaikolojia waliyo yapata watoto hao kwa kipindii chote baba yao alipo kuwa anaitwa gaidi?! Ni binadamu mwenye roho ya aina gani anaweza kuwa na furaha huku akijua kuwa watoto
wako wanaumia na kuteseka?

4. Ni binadamu wa aina gani anayeweza kuandaa shutma za uongo na
kuwaaminisha watanzania kuwa
niza kweli huku akimtaja Mungu kuwa anaweza kumpelekea ushahidi wake?! Na tangu lini Mungu akawa na shufaa ya kupokea ushahidi kutoka kwa
wanadamu twenye mapungufu na maadhaifu lukuki mbali na mitume walio kuwa wanapewa maagizo na Mungu kwa njia ya kuoteshwa?!

5. Imeandikwa, "mpende jirani yako kama unavyoipenda nafsi
yako" ikaandikwa tena "Usimshuhudie
mwenzako uongo", Mwigulu anasali kanisa gani ambalo hakuwahi kupata mafundisho haya?!, na ni binadamu wa aina
gani anaye yafanya haya huku akiwa amekusudia tena na kuapa ndani ya
nyumba inayopewa sifa ya utukufu?! Mtu huyu ana hofu ya Mungu ndani
yake?!

HITIMISHO.

Mimi namuona Mwigulu kama shetani kwa kuwa amekuwa na
mipango ya kishetani ambayo sasa
imekwama pamoja na ushetani wake. Na sasa ni wakati wa kumuombea aende ushetanini akapeleke ushahidi wake maana umeshindikana hapa duniani penye macho ya binadamu wenzake ambao ni wengi na kimsingi kuna kale kamsemo "Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu".

• Kumradhi kwa niliye mkwaza! Ni mtazamo na maono yangu.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...