Saturday, March 19, 2016

Bill Gates: Msomaji Makini wa Vitabu

Bill Gates, tajiri mkubwa kuliko wote duniani, ni msomaji makini wa vitabu. Anasoma vitabu yapata 50 kwa mwaka. Anaviona kuwa njia bora ya kujipatia elimu, hata kwa yule ambaye hakusoma sana shuleni. Yeye mwenyewe alijiunga kama mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Harvard, lakini alijiondoa bila kuhitimu.

Kwa maelezo yake mwenyewe, Bill Gates anasema kuwa tangu alipokuwa mtoto, alikuwa na ndoto nyingi kuhusu maisha yake ya baadaye. Anashukuru kwamba wazazi wake walimpa fursa tele za kusoma vitabu, ambavyo vilistawisha ndoto zake.

Sasa, katika utu uzima wake, anaendelea kusoma vitabu vya aina mbali mbali, ingawa anapenda zaidi vitabu vinavyoelimisha, kama vile vitabu vinavyoelezea mabadiliko ya dunia, sayansi, tekinolojia, na jamii, na namna binadamu anavyoweza kuchangia mabadiliko chanya. Anapenda vitabu vinavyohusu namna ya kutatua matatizo kama vile magonjwa.

Unaweza kujionea jinsi Bill Gates anavyovithamini vitabu ukitembelea blogu yake. Ziko pia video ambamo anaongelea vitabu, kwa mfano hii hapa.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...