Saturday, October 22, 2011

Ukiwa na Siri, Iweke Kitabuni

Hapa kuna picha nilizopiga kwenye tamasha la vitabu mjini Minneapolis, Oktoba 15, mwaka huu. Habari za tamasha hilo niliziandika hapa.

Picha zote hizi nilizipiga kwa muda wa dakika mbili hivi, nikiwa nimesimama sehemu moja.












Niliangalia jinsi watu walivyokuwa wanavichangamkia vitabu. Nilikumbuka ule usemi kuwa ukiwa na siri, iweke kitabuni. Hapo watu makini na wasio makini watajipambanua wenyewe.









Kwa uzoefu wangu, kama ninavyosema tena na tena katika blogu na sehemu zingine, wa-Marekani ni kati ya hao watu makini. Ukiweka siri kitabuni, wataiona.






No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...