Saturday, February 25, 2012

Picha za Wadau Wakiwa na Vitabu

Hapa naleta picha niizopiga na wadau mbali mbali wa vitabu vyangu. Kila picha inanikumbusha tukio la kukutana na wadau hao. Kila picha inabeba historia fulani, na ningeweza kuisimulia. Kitu kimoja kinachonifikirisha ni jinsi watu wanavyoshika vitabu wakat wa kupigwa picha. Karibu wote wanaweka kitabu sehemu ya kifuani, karibu na moyoni, na wengine karibu na tumboni. Mtu unaweza kuandika insha kuhusu suala hilo, kuelezea saikolojia inayoandamana na upigaji picha kwa upande wa mpiga picha na mpigwa picha, kama watafiti wengine walivyofanya, halafu ukajikita katika kuwaelezea hao wadau wanaopigwa picha wakiwa wameshika vitabu vyao.

Hapa ni mjini Faribault, Minnesota, wakati wa tamasha la tamaduni mbali mbali.












Hapa ni Sinza, Dar es Salaam. Huyu mdau ni Gilbert Mahenge, mwanakijiji wa Msoga, Bagamoyo. Huyu ni kati ya wa-Tanzania wachache ambao nawaona wameelimika kiukweli, kwa maana kwamba anatafuta elimu bila kuchoka. Mara ya kwanza kukutana naye, tulikuwa kwenye basi tukitokea Dar es Salaam. Katika begi lake alikuwa na vitabu. Hapo Sinza pia, tulipokutana tena, alikuwa na vitabu, hata akaniulizia kuhusu kitabu fulani ambacho sikuwa nimekisikia. Yeye alishakisoma. Hasomi kwa sababu ya mitihani, bali kwa kujielimisha.

Hiyo ni familia ya ki-Jerumani. Tulipiga picha hii kituo cha mabasi Ubungo, Dar es Salaam, wakati wao walipokuwa wanasafiri kwenda Ruvuma, ambako alizaliwa huyu mama wa familia, aliye pembeni yangu.









Hapa ni Brooklyn Park, Minnesota, kwenye tamasha la nchi za ki-Afrika. Huyu wa katikati ni mdau Richard Fillie kuoka Sierra Leone. Alimleta huyu mwingine, ambaye anatoka Sudan. Staili yao ya kushika vitabu ni tofauti na ya wengine.








Hapa ni viwanja vya makumbusho ya Taifa, Dar es Salaam, Septemba, 2004, wakati wa tamasha la vitabu. Niko na dada yangu na mdau Eiko Kimura kutoka Japani.









Hapa ni ndani ya maktaba ya Chuo cha St. Olaf. Huyu kijana ni mwanafunzi.













Hapa ni Minneapolis, Minnesota, kwenye mkutano wa watu wenye asili ya Afrika. Huyu mdau naye ni mwandishi M. Ann Pritchard.

















Hapa ni Madison, Wisconsin, nyumbani kwa mwalimu Wade Dallagrana, huyu aliyeshika kitabu.












Hapa ni viwanja vya makumbusho ya Taifa, Dar es Salaam, Septemba, 2004, wakati wa tamasha la vitabu. Niko na mdau kutoka Japani. Yeye amevisogeza vitabu karibu na kifua changu.















Hapa ni viwanja vya makumbusho ya Taifa, Dar es Salaam, Septemba 2004, wakati wa tamasha la vitabu. Niko na dada yangu na wadau wa Canada.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...