Wednesday, February 29, 2012

Wadau Walionitembelea "Danish," Arusha

Mwaka 2007, nilikuwa Tanzania na wanafunzi na mwalimu mmoja kutoka Chuo cha Colorado waliokuja kwenye kozi yangu ya Hemingway in East Africa. Ni kozi ya wiki tatu. Tulifika na kuanzia kozi kwenye kituo cha "Danish," Arusha, wiki ya mwisho ya Mei.

Kama ilivyo kawaida ninapokuwa Tanzania, wadau mbali mbali hunitafuta. Basi hapo Danish alikuja Mama Esther Simba, mwenye gauni jekundu pichani, na rafiki yake, ambaye jina lake limenitoka.

Tulikuwa tumewasiliana kwa kitambo, kwa barua pepe. Yeye alikuwa mshauri katika programu ya Cross Cultural Solutions, ambayo inaleta watu wa kujitolea Tanzania. Alikuwa anawapokea na kuwahudumia, pamoja na kuwaelimisha kuhusu maisha na utamaduni wa Tanzania.

Mama Simba ni mdau wa kitabu changu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences. Shughuli zetu zinahusiana vizuri, kwani nami huwaelimisha wa-Marekani kuhusu utamaduni wa wa-Afrika, na pia nawaelimisha wa-Afrika kuhusu utamaduni wa wa-Marekani chini ya kampuni ya Africonexion.

Kukutana na wadau namna hiyo ni fursa nzuri ya kubadilishana mawazo. Unaweza kumsikiliza Mama Simba anavyoelezea kwa ufasaha kabisa shughuli na manufaa ya Cross Cultural Solutions hapa.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...