Thursday, February 16, 2012

Tamasha la Vitabu, Houston

Kila mwaka kunafanyika tamasha la vitabu mjini Houston, liitwalo National Black Book Festival. Ni tamasha linalowajumuisha waandishi, wachapishaji na wauzaji wa vitabu, klabu za wasoma vitabu, wahudumu wa maktaba, na wadau wengine wengi. Wanapata fursa ya kukutana na kufahamiana, kuongelea masuala mbali mbali yanayohusu vitabu.

Nimeshiriki tamasha la vitabu Minneapolis kwa miaka kadhaa, kama nilivyoandika hapa na hapa. Mimi hushiriki kama mwandishi wa vitabu hivi hapa. Hili tamasha la Houston nimelifahamu kwa miaka kadhaa, kwa kusoma taarifa zake. Kwa miaka yapata miwili iliyopita, nimekuwa nikiwazia kushiriki tamasha hilo.

Sio lazima niende mwenyewe Houston au kila mahali kwenye shughuli kama hizi. Ingekuwa nina washirika, kama nilivyodokeza katika blogu hii, wangeweza kuniwakilisha, kama nilivyowakilishwa na wadau wa utalii Mto wa Mbu katika maonesho ya utalii Arusha. Yote hiyo ni mipango ya kuitafakari na changamoto za kuzifanyia kazi. Penye nia pana njia, wala hakuna wasi wasi.

No comments:

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...