
Showing posts with label CCM. Show all posts
Showing posts with label CCM. Show all posts
Monday, September 28, 2015
Kampeni za CCM Mwaka Huu

Tuesday, December 9, 2014
Uhuru wa Tanganyika na Ukoloni Mamboleo

Uhuru tulipata tarehe 9 Desemba, 1961. Nilikuwa mwanafunzi wa darasa la tatu, na ninakumbuka msisimko, hata kule kijijini kwangu. Waalimu wetu, Charles Kinunda, John Pantaleon Mbonde, na Alois Turuka, walikuwa chanzo kikubwa cha ufahamu wetu wa mambo yaliyokuwa yanatokea.
Kati ya kumbukumbu ambazo haziwezi kutoweka akilini mwangu ni picha ya askari Alexander Nyirenda akiweka mwenge wa Uhuru juu ya Mlima Kilimanjaro. Sambamba na tukio hili la kihistoria ni hotuba ya Mwalimu Julius Nyerere, ambamo alisema:
Sisi tunataka kuwasha mwenge, na kuuweka juu ya Mlima Kilimanjaro, ili umulike hata nje ya mipaka yetu, ulete tumaini pale ambapo hakuna matumaini, upendo mahali palipo na chuki, na heshima palipojaa dharau.


Hayo yote, tangu enzi za harakati za Uhuru hadi miaka ya mwisho mwisho ya sabini na kitu, yalifanyika chini ya uongozi wa chama cha TANU. Mtazamo na mwelekeo wa TANU ulikuwa wa kuongoza mapinduzi, kufuatana na mazingira ya kihistoria: kwanza ilikuwa kuwaunganisha wa-Tanganyika na kuwaongoza katika kupigania Uhuru, halafu, kuongoza harakati za kujenga ujamaa na kujitegemea.
Mwalimu Nyerere alifahamu fika kwamba Uhuru haukuwa mwisho wa safari. Kulikuwa na haja ya kupambana na urithi wa ukoloni, yaani ukoloni mamboleo na kuleta uhuru wa kweli, unaodhihirishwa na hali ya kujitegemea chini ya uongozi bora.
Miaka ilivyopita, baada ya chama kipya cha CCM kushika hatamu, hali ilikuwa hiyo kwa kipindi cha mwanzo. Lakini, pole pole, mwelekeo huu wa kuwa daima katika harakati za mapinduzi, ulianza kubadilika. Chini ya sera za CCM, kama vile "Azimio la Zanzibar," nchi imeendelea kuzama zaidi na zaidi katika mfumo wa matabaka na ukoloni mamboleo. Kwa lugha rahisi, CCM ni mhujumu wa Mapinduzi.
Ndoto na mategemeo ya Uhuru yametekwa nyara. Pamoja na kwamba tunasherehekea Uhuru tuliojipatia mwaka 1961, tutambue, kama TANU ilivyotambua, kuwa ule haukuwa mwisho wa safari. Enzi za TANU, tulitegemea kuwa tutajenga nchi ambayo iko chini ya mamlaka ya wakulima na wafanyakazi. Lakini, kama nilivyosema hapa juu, tunazidi kuzama katika ukoloni mamboleo. Wakulima na wafanyakazi, pamoja na washiriki wao, bado wana jukumu la kuendeleza harakati za kutafuta Uhuru wa kweli.
Tuesday, April 5, 2011
Mwalimu Nyerere Aongelea Uongozi, 1995
Suala la uongozi lilikuwa moja ya vipaumbele vya Mwalimu Nyerere maisha yake yote. Tunasikia, kwa mfano, jinsi alivyolichukulia suala hili alipokuwa kiongozi wa wanafunzi katika shule ya Tabora. Wakati wa kupigania Uhuru na baada ya Uhuru aliliongelea suala hili tena na tena, kama vile katika "Azimio la Arusha" na "Mwongozo."
Mwalimu aliliongelea suala hili tena, kwa masikitiko, katika kitabu chake cha "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania," akiihofia hatima ya Tanzania kutokana na uongozi mbovu wa CCM. Niligusia suala hilo katika makala hii hapa. Hata baada ya kuandika kitabu hiki, Mwalimu aliendelea kuongelea suala la uongozi. Hebu msikilize katika hotuba yake hii ya mwaka 1995.
Mwalimu aliliongelea suala hili tena, kwa masikitiko, katika kitabu chake cha "Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania," akiihofia hatima ya Tanzania kutokana na uongozi mbovu wa CCM. Niligusia suala hilo katika makala hii hapa. Hata baada ya kuandika kitabu hiki, Mwalimu aliendelea kuongelea suala la uongozi. Hebu msikilize katika hotuba yake hii ya mwaka 1995.
Friday, November 19, 2010
Wabunge wa CCM Wanakera
Wabunge wa CCM wanakera. Tukianzia na wabunge hao walioapishwa safari hii, sitasahau kuwa hao ndio waheshimiwa waliotoroka midahalo wakati wa kampeni. Wote walitoroka midahalo, kitendo ambacho kimenikera. Mimi kama mwalimu, ninayetambua umuhimu wa midahalo, ninawashutumu hao waheshimiwa. Soma hapa.
Kila nitakapokuwa naona sura za hao waheshimiwa wa CCM, nitakuwa nakumbuka kitendo chao hiki cha kutoroka midahalo. Nitakuwa naangalia kama watajirekebisha au kama kitendo kile ni ishara ya tabia na mwenendo watakaofuata kwa miaka mitano ijayo.
Tukirudi nyuma, kwenye awamu iliyopita, wabunge wa CCM walikera. Ni nani atakayesahau yaliyotokea wakati Dr. Slaa alipoanza kutamka kuwa kuna ufisadi katika nchi yetu? Wabunge wote wa CCM walimpinga vikali na kumtupia shutuma nzito kwamba alikuwa mzushi.
Dr. Slaa hakuyumba, bali aliendelea kutoa madai yake. Hatimaye, ilianza kuthibitika kuwa aliyokuwa anayasema ni kweli, kwamba tuna mafisadi. Baada ya wananchi kuanza kuona ukweli huo, ukawa haupingiki tena, tuliwaona baadhi ya wabunge wa CCM wakijitokeza na kuanza kujinadi kuwa nao ni wapiganaji dhidi ya ufisadi. Sijui kama walikuwa wanaongea kwa dhati au kwa lengo jingine.
Tukirudi nyuma zaidi, tunakumbuka suala la machafuko yaliyotokea Visiwani mwaka 2001. Machafuko yale, yaliyotokana na CCM, chama tawala, kushindwa kutumia haki na busara, yaliiletea Tanzania aibu kubwa duniani. Kwa uthibitisho, soma hapa.
Lakini, pamoja na maovu yote yaliyofanyika Visiwani, pamoja na fedheha yote iliyoiangukia Tanzania, wabunge wa CCM hawakukubali kuwa serikali ya CCM ilikuwa na makosa, wala hawakukubali kuwa Tanzania ilikuwa inafedheheka. Wao waliitetea serikali ya CCM. Maadam palikuwa na suala lililohusu chama cha upinzani, yaani CUF, wabunge wa CCM waliamua kuikingia kifua serikali ya CCM, badala ya kusimamia haki za binadamu na heshima ya Tanzania.
Je, kuna kero kubwa zaidi ya hii ya kutojali maslahi ya Taifa na badala yake kuangalia maslahi ya kikundi fulani?
Kila nitakapokuwa naona sura za hao waheshimiwa wa CCM, nitakuwa nakumbuka kitendo chao hiki cha kutoroka midahalo. Nitakuwa naangalia kama watajirekebisha au kama kitendo kile ni ishara ya tabia na mwenendo watakaofuata kwa miaka mitano ijayo.
Tukirudi nyuma, kwenye awamu iliyopita, wabunge wa CCM walikera. Ni nani atakayesahau yaliyotokea wakati Dr. Slaa alipoanza kutamka kuwa kuna ufisadi katika nchi yetu? Wabunge wote wa CCM walimpinga vikali na kumtupia shutuma nzito kwamba alikuwa mzushi.
Dr. Slaa hakuyumba, bali aliendelea kutoa madai yake. Hatimaye, ilianza kuthibitika kuwa aliyokuwa anayasema ni kweli, kwamba tuna mafisadi. Baada ya wananchi kuanza kuona ukweli huo, ukawa haupingiki tena, tuliwaona baadhi ya wabunge wa CCM wakijitokeza na kuanza kujinadi kuwa nao ni wapiganaji dhidi ya ufisadi. Sijui kama walikuwa wanaongea kwa dhati au kwa lengo jingine.
Tukirudi nyuma zaidi, tunakumbuka suala la machafuko yaliyotokea Visiwani mwaka 2001. Machafuko yale, yaliyotokana na CCM, chama tawala, kushindwa kutumia haki na busara, yaliiletea Tanzania aibu kubwa duniani. Kwa uthibitisho, soma hapa.
Lakini, pamoja na maovu yote yaliyofanyika Visiwani, pamoja na fedheha yote iliyoiangukia Tanzania, wabunge wa CCM hawakukubali kuwa serikali ya CCM ilikuwa na makosa, wala hawakukubali kuwa Tanzania ilikuwa inafedheheka. Wao waliitetea serikali ya CCM. Maadam palikuwa na suala lililohusu chama cha upinzani, yaani CUF, wabunge wa CCM waliamua kuikingia kifua serikali ya CCM, badala ya kusimamia haki za binadamu na heshima ya Tanzania.
Je, kuna kero kubwa zaidi ya hii ya kutojali maslahi ya Taifa na badala yake kuangalia maslahi ya kikundi fulani?
Thursday, October 28, 2010
Mgombea wa CCM Kufanya Mahojiano
Zikiwa zimebaki siku tatu tu hadi uchaguzi ufanyike nchini Tanzania, tumepata habari kuwa mgombea urais kwa tiketi ya CCM atafanya mahojiano na vyombo vya habari. Hii ni tofauti na msimamo wa CCM katika kipindi chote cha kampeni, ambapo wagombea wake walikuwa hawashiriki midahalo.
Wengi wetu tunafahamu kuwa midahalo, mahojiano, na kadhalika, ni mambo muhimu katika jamii inayothamini elimu. Sasa kwa nini CCM haikutambua hilo kabla? Tena CCM ni chama chenye wanachama milioni kadhaa, wakiwemo "wasomi" wengi.
Ni lazima niulize: hao ni wasomi kweli au ni wababaishaji? Ni aibu kuwa hawakuweza kuchangamka kabla na kutambua umuhimu wa midahalo, hadi saa hii ya mwisho, na baada ya Dr. Slaa kuonyesha mfano.
Mimi kama mwalimu, na pia raia ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nawajibika kuwashutumu CCM kwa kutoonyesha mfano bora, pale walipotamba kuwa mgombea wao hahitaji kushiriki midahalo. Na pamoja na hayo, wagombea wao wote wakawa hawashiriki midahalo. Sijui kama ilikuwa ni fikra zao au ndio nidhamu ya chama. Kama ndio nidhamu ya chama, ni heri nibaki bila chama, kuliko kuwa katika himaya ya udikteta.
Narudia kuushutumu uamuzi wa kutoshiriki midahalo. Na hao wagombea wote nawashutumu kwa kutii amri isiyo na busara kama hiyo. Je, sasa, kwa vile JK ameamua kufanya mahojiano, nao watakimbilia kwenye vyombo vya habari kufanya mahojiano? Akili gani hiyo? Mimi kama mwalimu, lazima niulize: tunawafundisha nini watoto wetu, ambao ni taifa la kesho?
Baada ya kusema hayo, mimi kama raia mwema, ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nina masuali kwa mgombea wa CCM. Kwa vile hakuna muda wa kuuliza yote, nitauliza matatu tu.
La kwanza ni kwa nini wale ambao Dr. Slaa amewataja katika orodha yake ya mafisadi hawajampeleka mahakamani hadi leo?
La pili ni je, kwa nini CCM inadai kuwa amani Tanzania inatokana na uongozi wa CCM, wakati CCM inashiriki kikamilifu katika kuhujumu amani, hasa nyakati za kampeni na uchaguzi? Mifano ni mingi, kuanzia Visiwani hadi Bara, na hata ripoti za kimataifa zinathibitisha hilo. Kwa mfano, soma hapa na pia angalia video hizi hapa.
Ukweli ni kitu muhimu sana. Je, CCM haitambui kuwa wanaotunza amani Tanzania kikweli kweli ni sisi mamilioni ya raia ambao si wanachama wa chama chochote cha siasa? Hatuna rekodi yoyote ya kuvuruga amani kama wenzetu wenye vyama wanavyofanya. Kwa nini CCM inafunika ukweli huo?
Suali la tatu ni je, CCM ina maelezo gani kuhusu shutuma alizotoa Mwalimu Nyerere dhidi ya CCM katika kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania? Kuzifahamu kwa ufupi shutuma hizi, soma hapa.
Wengi wetu tunafahamu kuwa midahalo, mahojiano, na kadhalika, ni mambo muhimu katika jamii inayothamini elimu. Sasa kwa nini CCM haikutambua hilo kabla? Tena CCM ni chama chenye wanachama milioni kadhaa, wakiwemo "wasomi" wengi.
Ni lazima niulize: hao ni wasomi kweli au ni wababaishaji? Ni aibu kuwa hawakuweza kuchangamka kabla na kutambua umuhimu wa midahalo, hadi saa hii ya mwisho, na baada ya Dr. Slaa kuonyesha mfano.
Mimi kama mwalimu, na pia raia ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nawajibika kuwashutumu CCM kwa kutoonyesha mfano bora, pale walipotamba kuwa mgombea wao hahitaji kushiriki midahalo. Na pamoja na hayo, wagombea wao wote wakawa hawashiriki midahalo. Sijui kama ilikuwa ni fikra zao au ndio nidhamu ya chama. Kama ndio nidhamu ya chama, ni heri nibaki bila chama, kuliko kuwa katika himaya ya udikteta.
Narudia kuushutumu uamuzi wa kutoshiriki midahalo. Na hao wagombea wote nawashutumu kwa kutii amri isiyo na busara kama hiyo. Je, sasa, kwa vile JK ameamua kufanya mahojiano, nao watakimbilia kwenye vyombo vya habari kufanya mahojiano? Akili gani hiyo? Mimi kama mwalimu, lazima niulize: tunawafundisha nini watoto wetu, ambao ni taifa la kesho?
Baada ya kusema hayo, mimi kama raia mwema, ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, nina masuali kwa mgombea wa CCM. Kwa vile hakuna muda wa kuuliza yote, nitauliza matatu tu.
La kwanza ni kwa nini wale ambao Dr. Slaa amewataja katika orodha yake ya mafisadi hawajampeleka mahakamani hadi leo?
La pili ni je, kwa nini CCM inadai kuwa amani Tanzania inatokana na uongozi wa CCM, wakati CCM inashiriki kikamilifu katika kuhujumu amani, hasa nyakati za kampeni na uchaguzi? Mifano ni mingi, kuanzia Visiwani hadi Bara, na hata ripoti za kimataifa zinathibitisha hilo. Kwa mfano, soma hapa na pia angalia video hizi hapa.
Ukweli ni kitu muhimu sana. Je, CCM haitambui kuwa wanaotunza amani Tanzania kikweli kweli ni sisi mamilioni ya raia ambao si wanachama wa chama chochote cha siasa? Hatuna rekodi yoyote ya kuvuruga amani kama wenzetu wenye vyama wanavyofanya. Kwa nini CCM inafunika ukweli huo?
Suali la tatu ni je, CCM ina maelezo gani kuhusu shutuma alizotoa Mwalimu Nyerere dhidi ya CCM katika kitabu chake cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania? Kuzifahamu kwa ufupi shutuma hizi, soma hapa.
Wednesday, October 6, 2010
Chukua Chako Mapema
Pale CCM ilipoanzishwa, baadhi ya wa-Tanzania walianzisha minong'ono wakitafsiri CCM kama "Chukua Chako Mapema."
Nilitaja jambo hilo katika makala fupi, "Jokes Play Social Role," ambayo ilichapishwa katika gazeti la Daily News (Tanzania) (Juni 16, 1987) ukurasa 4.
Ni miaka mingi imepita, na ushahidi wa nini hasa maana ya CCM umeendelea kujitokeza. Tumsikilize katibu mkuu wa CCM:
Nilitaja jambo hilo katika makala fupi, "Jokes Play Social Role," ambayo ilichapishwa katika gazeti la Daily News (Tanzania) (Juni 16, 1987) ukurasa 4.
Ni miaka mingi imepita, na ushahidi wa nini hasa maana ya CCM umeendelea kujitokeza. Tumsikilize katibu mkuu wa CCM:
Friday, October 1, 2010
Mwalimu Nyerere Aliongelea Uozo Katika CCM
Mwalimu Nyerere aliongelea uozo katika CCM. Kwa mfano, wakati alipokuwa anajiandaa kung'atuka uenyekiti wa CCM, alizunguka nchi nzima akikagua uhai wa CCM. Wakati wa ziara hiyo, inaonekana Mwalimu alitatizwa na yale aliyoyaona. Aliwahi kusema kuwa kuna watu ndani ya CCM ambao hata mtihani juu ya Azimio la Arusha hawawezi kupasi.
Mwaka 1993 Mwalimu alichapisha kitabu kiitwacho Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (Harare: Zimbabwe Publishing House, 1993). Pamoja na mambo mengine katika kitabu hiki, Mwalimu alisema kuwa kuna kansa katika uongozi wa CCM. Nanukuu baadhi ya maneno yake:
Chama cha Mapinduzi, kwa sababu ya uzito wa historia yake, hadhi ya jina lake, mfumo wa wavu wake, mazoea ya watu, na ubovu wa Vyama vya Upinzani, kinaweza kuchaguliwa na Watanzania, pamoja na kansa ya uongozi wake. Au watu wanaweza wakachoka, wakasema, "potelea mbali:" wakachagua Chama cho chote, ilimradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM. Hainifurahishi kuyasema haya, lakini uhai wa Nchi yetu unataka yasemwe. (Ukurasa 61)
Mwalimu hakuishia hapo, bali aliongezea namna hii:
Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa Vyama Vingi. Nilitumaini kuwa tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha Chama cha Mapinduzi kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao. Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani; na wala dalili zo zote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama cha Mapinduzi, Chama hiki kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini hili si jambo la kutarajia bila hofu na wasi wasi! (Ukurasa 66)
Mwalimu Nyerere aliongelea hayo miaka yapata ishirini iliyopita. Leo hali ikoje? Kwa mtazamo wangu, uozo aliosemea Mwalimu umeongezeka. Hayo yamekuwa mawazo yangu tangu zamani. Kwa mfano, soma hapa.
Mwaka 1993 Mwalimu alichapisha kitabu kiitwacho Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (Harare: Zimbabwe Publishing House, 1993). Pamoja na mambo mengine katika kitabu hiki, Mwalimu alisema kuwa kuna kansa katika uongozi wa CCM. Nanukuu baadhi ya maneno yake:
Chama cha Mapinduzi, kwa sababu ya uzito wa historia yake, hadhi ya jina lake, mfumo wa wavu wake, mazoea ya watu, na ubovu wa Vyama vya Upinzani, kinaweza kuchaguliwa na Watanzania, pamoja na kansa ya uongozi wake. Au watu wanaweza wakachoka, wakasema, "potelea mbali:" wakachagua Chama cho chote, ilimradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM. Hainifurahishi kuyasema haya, lakini uhai wa Nchi yetu unataka yasemwe. (Ukurasa 61)
Mwalimu hakuishia hapo, bali aliongezea namna hii:
Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona Chama kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa Vyama Vingi. Nilitumaini kuwa tunaweza kupata Chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza Nchi yetu badala ya CCM; au ambacho kingekilazimisha Chama cha Mapinduzi kusafisha uongozi wake, kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao. Lakini bado sijakiona Chama makini cha upinzani; na wala dalili zo zote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama cha Mapinduzi, Chama hiki kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini hili si jambo la kutarajia bila hofu na wasi wasi! (Ukurasa 66)
Mwalimu Nyerere aliongelea hayo miaka yapata ishirini iliyopita. Leo hali ikoje? Kwa mtazamo wangu, uozo aliosemea Mwalimu umeongezeka. Hayo yamekuwa mawazo yangu tangu zamani. Kwa mfano, soma hapa.
Subscribe to:
Posts (Atom)
Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...

-
Leo ni kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwangu, ambayo ni tarehe 17 Agosti, 1951. Familia yangu, ndugu, na marafiki wamejumuika nami kushereh...
-
Kutafsiri kazi ya fasihi ni kazi ngumu ya kuchemsha bongo. Inahitaji ufahamu wa hali ya juu wa lugha husika, na pia hisia makini za kifasih...
-
Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...