Tuesday, June 30, 2015

Mambo ya Tamasha la Vitabu Mankato

Kila tamasha la vitabu au utamaduni ninaloshiriki huwa na mambo mengi ya kuelimisha na kuburudisha akili. Kukutana na watu na kuongea nao ni sababu muhimu ya ushiriki wangu katika matamasha hayo. Juzi katika tamasha la Deep Valley Book Festival, binti yangu Zawadi nami, tunaoonekana pichani hapa kushoto, tulikutana na kuongea na watu mbali mbali.

Kati ya hao alikuwepo mama mmoja ambaye si rahisi kumsahau. Alifika mezani petu, na wakati tunasalimiana alinyanyua nakala ya Matengo Folktales, Africans and Americans: Embracing Cultural Differences, Notes on Achebe's Things Fall Apart, na Africans in the World, akasema anavinunua.

Wakati wote alikuwa anatuelezea kuwa alikuwa na binti yake ambaye aliishi China kwa miaka nane kisha akaenda Namibia, na kwamba ameipenda Namibia tangu  mwanzo. Alituambia tumwekee vitabu vyake, na kwamba binti yake angefika baadaye.

Yapata nusu saa kabla ya tamasha kwisha, huyu binti alikuja. Tuliongea naye, akatuambia jinsi alivyoipenda Namibia akifananisha na China. Mama yake naye akaja. Akaulizia vile vitabu tulivyomwekea, tukavichukua chini ya meza tulipovihifadhi, tukampa. Aliziangalia "t-shirt," akainyanyua moja na kuilipia. Kwa kuwa alinunua vitu vyote hivi: vitabu vinne na "t-shirt," tulimpunguzia bei, ingawa hakutegemea. Tulisahau kupiga picha pamoja naye na binti yake, kwa kumbukumbu.

Huyu mama hapa kulia ni mwalimu Becky Fjelland Davis wa Chuo cha South Central, Mankato. Ni mpenzi wa kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences na mpiga debe wake mkuu. Nami nilinunua kitabu chake, Jake Riley: Irreparably Damaged.

Huyu mwenzake alijitambulisha kwangu na binti yangu hiyo jana, akasema kwamba alihudhuria mhadhara wangu Chuoni South Central, "Writing About Americans." Huku akiusifia mhadhara ule, alinunua kitabu cha Africans and Americans: Embracing Cultural Differences.


Nimeona niiongelee tena picha hiyo hapa kushoto, ingawa nilishaigusia juzi. Huyu mama ni Becky, ambaye nimemwongelea hapa juu. Huyu bwana, Paul Dobratz, ambaye alikuwa katika msafara wa Becky wa Afrika Kusini, alitusisimua, akishirikiana na Becky, kwa habari kem kem na michapo ya safari yao.

Hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Paul kwenda Afrika, lakini Afrika iliuteka moyo wake kiasi kwamba anataka kwenda tena. Nimekutana au kuwasiliana na wa-Marekani wengi ambao wakishafika Afrika wanatekwa mioyo hivi hivi. Mwandishi Ernest Hemingway alikumbwa na hali hiyo wakati alipokuwa akizunguka Tanganyika mwaka 1933-34, kama alivyoandika katika Green Hills of Africa. Yeye na mke wake Pauline walijawa na hisia za kuipenda sana Tanganyika, kiasi kwamba hawakupenda kuondoka. Kwa maneno yake mwenyewe: "We had not left it, yet, but when I would wake in the night I would lie, listening, homesick for it already.”

Sunday, June 28, 2015

Tamasha la Vitabu Mankato Limefana

Leo, nikiwa na binti yangu Zawadi, tulikwenda Mankato kushiriki tamasha la vitabu, Deep Valley Book Festival. Niliandika habari za tamasha hilo katika blogu yangu ya ki-Ingereza. Nilipeleka vitabu vyangu vinavyoonekana mtandaoni, pamoja kijitabu kiitwacho Africans in the World. Vile vile tulipeleka "t-shirt" kama hizo tulizovaa pichani, zenye nembo ya kampuni yangu ndogo Africonexion: Cultural Consultants. Tunajifunza mengi katika kukutana na watu wanaofika kwenye meza yetu. Hatujui nini kitamvutia mtu fulani na kwa nini. Lakini watu hujieleza. Tunasikia habari nyingi, nyingine za kushangaza, zinazomfanya mtu anunue hiki au kile.

Inatufurahisha kuwaangalia watu wakipita kwenye meza mbali mbali kuangalia vitabu, kuongea na waandishi, wachapishaji na wengine wanaokutana nao katika tamasha. Nasi tunapata fursa ya kukutana na watu mbali mbali. Leo, kwa mfano, wamefika watu kwenye meza yetu ambao wametuambia wamefika Afrika: Botswana, Tanzania, na Namibia. Tunahisi walivutiwa na "t-shirt" tulizovaa, zenye ya ramani ya Afrika. Kila mmoja ametusimulia habari za safari yake. Tulijua kuwa tutakutana na baadhi ya watu tuliokutana nao wakati nilipotoa mihadhara katika Chuo cha South Central, katika maandalizi ya safari ya Afrika Kusini. Kama tulivyotarajia, walikuwepo watu kadhaa.



Hapa kushoto anaonekana kiongozi wa safari ya Afrika Kusini, mwalimu Becky Fjelland Davis, ambaye ni mwandishi. Alishiriki tamasha. Mwingine ni Paul Dobratz ambaye alihudhuria shughuli zote nilizofanya wakati wa ziara yangu Chuoni South Central. Naye alikuwemo katika safari ya Afrika Kusini. Binti yangu nami tulifurahi sana kusikia habari za safari.




Kama ilivyo kawaida hapa Marekani, watu wa rika mbali mbali huhudhuria matamasha haya ya vitabu. Wanayathamini sana, na mahudhurio huwa makubwa.

Daima ninaguswa ninapowaona wazazi wakiwa na watoto wao. Ninaguswa na jinsi wanavyowalea watoto wao katika utamaduni wa kupenda kusoma vitabu.






Imekuwa siku ya furaha sana kwa binti yangu na mimi. Tumefurahi kukutana na kuongea na watu wa aina aina, tuliowafahamu na ambao hatukuwafahamu. Tumerudi na kumbukumbu nyingi.

Thursday, June 25, 2015

Habari ya Malipo ya Mhadhara Chuoni Winona

Jumanne wiki hii, nilikwenda Chuo Kikuu cha Winona kutoa mhadhara, kama nilivyoandika katika blogu hii. Katika safari kama hii, kuna mambo mengi, na haiwezekani kuyaongelea yote. Hata hivi, naona ni vizuri tu kuelezea angalau yale yenye umuhimu Fulani kwangu na labda kwa wengine. Napenda kuongelea suala la malipo ya mhadhara ule.

Wakati nilipoombwa kwenda kutoa mhadhara, mhusika aliniuliza malipo yangu ni kiasi gani. Huu ni utaratibu hapa Marekani, nami kama ilivyo kawaida yangu, nilimwambia kuwa siweki kipaumbele kwenye malipo, bali kutoa huduma itakiwayo. Kama wanaonialika wana uwezo wa kunilipa, kwangu ni sawa, kama wana uwezo kidogo, kwangu ni sawa, na kama hawana uwezo, kwangu ni sawa pia. Niko tayari kuitikia mwito kwa hali yoyote. Nilidhani suala lilikuwa limeishia hapo.

Siku kadhaa baadaye, mhusika alinielezea tena habari ya malipo, akataja kiasi ambacho angeweza kunilipa, kutokana na bajeti yake. Nilimjibu kuwa sina tatizo, nikamshukuru. Alipoleta mkataba, ambao ulitaja kiasi hicho cha malipo, niliusaini bila kusita, nikamrudishia.

Siku ilipofika, yaani hiyo tarehe 23 Juni, binti yangu Zawadi nami tulikwenda Chuoni Winona. Tulikaribishwa vizuri, tukaingia kwenye ukumbi wa mkutano wakati huo huo wanafunzi walipokuwa wanaingia. Baada ya kila mtu kuketi, mwenyeji wangu alisimama kunitambulisha. Alisema tunaye mgeni hapa, Dr. Mbele, profesa wa Chuo cha St. Olaf. Ni mtu ambaye nimemfahamu kwa miaka kadhaa, na nimemwomba aje atoe mhadhara.

Hadi hapo, sikuona kitu cha pekee, kwani huo ni utaratibu wa kawaida. Kilichokuwa cha pekee ni pale alipoanza kuelezea mazungumzo yetu juu ya malipo. Aliwaambia wanafunzi kuwa Dr. Mbele aliniambia kuwa hajali kama nina malipo kiasi gani ya kumpa, angekuja tu. Nasikitika kuwa kiasi nilichoweza kumwekea hakifanani na umaarufu wake. Niko njiani kutafuta hela kwa program nyingine, niweze kumwalika na kumlipa kiwango anachostahili.

Kwa kweli, sikutegemea angesema yote hayo, na nilimsikiliza kwa kumhurumia kwa jinsi alivyoonekana kujisikia vibaya kwamba ameshindwa kunitayarishia malipo ninayostahili. Nilifarijika alipomaliza maelezo yake na kunikaribisha nitoe mhadhara.

Baada ya mhadhara, mwenyeji wangu aliniongoza kwenda ofisini kwake, akanipa fomu ya malipo nisaini. Kisha akanipa cheki. Nilishangaa kuona cheki ilikuwa imezidi kile kiwango alichoniambia mwanzo. Nikaona kuwa alikuwa amejitahidi alivyoweza kuvuka kile kiwango tulichokubaliana. Na bado aliendelea kulalamika kuwa angeridhika kama angenilipa ninavyostahili.

Nimeona niongelee jambo hili, kwani ni kati ya mambo ambayo sitayasahau. Pia ni jambo lenye maana kwangu. Nimetamka tena na tena kuwa siweki pesa mbele, bali huduma. Hata hivi, ninafahamu jinsi wa-Marekani wanavyojali malipo. Wanazingatia umuhimu wa kumlipa mtu kile wanachoona ni haki yake.

Ningeweza kusema kuwa ninapaswa kuzingatia umuhimu wa kufuata utamaduni wa mahali nilipo. Lakini suala hili la malipo bado ni mtihani kwangu, kama nilivyowahi kuandika katika blogu hii. Ninaamini kuwa kwa kuzingatia huduma kwa wanadamu, badala ya ubinafsi, sipotezi chochote. Badala yake, Mungu ananibariki. Ninaishi na raha moyoni. Ninafurahi kwamba binti yangu alishuhudia yote niliyoeleza hapo juu. Labda yatamsaidia maishani.

Wednesday, June 24, 2015

Uzinduzi wa Filamu ya "Papa's Shadow"

Jana ilikuwa siku ya pekee kwangu. Nilihusika na matukio mawili muhimu sana, kama nilivyoripoti katika blogu hii. Napenda kuongelea tukio mojawapo: uzinduzi wa filamu ya "Papa's Shadow." Habari ya filamu hii nimezungumzia kabla katika blogu hii, lakini imeelezwa pia, vizuri kabisa, kwenye tovuti ya Ramble Pictures.

Jana ilikuwa siku tuliyoingojea kwa hamu kubwa. Ilikuwa ni siku ya kuonyeshwa filamu ya "Papa's Shadow" hadharani, ingawa wote walikuwa waalikwa. Kwa kuwa mimi ni mhusika mkuu katika filamu hiyo kama mzungumzaji sambamba na Mzee Patrick Hemingway, uwepo wangu ulikuwa muhimu.

Nilijikuta niko miongoni mwa kadamnasi iliyoniona maarufu. Nina hakika kuwa huu utakuwa mzigo maishani, kwani nitategemewa kujua mengi juu ya Hemingway kuliko inavyowezekana. Hiyo jana tu masuali magumu yalikuwa yanaelekezwa kwangu. Hata hivi, hii ni changamoto nzuri ya mimi kuendelea kujielimisha.

Baada ya filamu kuonyeshwa, watu walikuja na kunishukuru sana kwa mengi niliyosema juu ya Hemingway. Mtu mmoja, kwa mfano, aliyejitambulisha kwangu kama mwalimu wa "high school," alinionyesha daftari ambamo alikuwa ameandika mambo yaliyomgusa zaidi katika filamu, na alisema kuwa amepata hamasa ya kuanza kusoma tena maandishi ya Hemingway.

Nilifurahi kuwa binti zangu walikuwepo kushuhudia uzinduzi. Kwa bahati mbaya mama yao hakuweza kujiunga nasi kwa kuwa alikuwa kazini.

Hapa kushoto niko na binti yangu wa kwanza, Deta, ambaye hajawa na fursa nyingi za kushuhudia shughuli zangu. Hii ni kutokana na majukumu ya kazi, sawa na mama yake. Lakini jana ilikuwa fursa nzuri, na sote tulifurahi.











Hapa kushoto niko na binti yangu wa pili, Assumpta. Huyu ndiye aliyeanzisha utani kuwa baada ya filamu hii ya "Papa's Shadow," nijiandae kutua Hollywood.

















Hapa kushoto niko na Zawadi binti yangu wa tatu. Huyu amekuwa akifuatana nami katika shughuli zangu tangu utoto wake. Anafahamu vizuri mawazo yangu, na anaweza kuniwakilisha katika matamasha bila mimi kuwapo.









Hapa kushoto tuko na Jimmy Gildea, mtengeneza filamu. Alikuwa mmoja wa wanafunzi 29 waliokuja Tanzania kwenye kozi yangu ya "Hemingway in East Africa," Januari, 2013.

Nimefanikiwa katika mambo mengi maishani, hasa katika masomo, na yote yameniletea furaha. Lakini nimefurahi zaidi kwa uzinduzi wa filamu hii na kwa jinsi nilivyowashirikisha watoto wangu. Waliyojionea na kuyasikia hiyo jana watayakumbuka.

Tuesday, June 23, 2015

Imekuwa Siku ya Mafanikio Makubwa

Leo imekuwa siku ya mafanikio makubwa. Kwanza nilienda Chuo Kikuu cha Winona na binti yangu Zawadi nikatoa mhadhara. Nilitumia hadithi za jadi kujadili namna wahenga wetu walivyozielewa dhana za uongozi na uwajibikaji.

Baada ya kuelezea kwa ufupi jinsi Afrika ilivyokuwa chimbuko la binadamu, lugha, sayansi, tekinolojia, na falsafa, nilisimulia hadithi mbili zilizomo katika kitabu changu cha Matengo Folktales, kuthibitisha namna wahenga wetu walivyoyatafakari masuala ya jamii. Hadithi hizo ni "The Monster in the Rice Field" na "Nokamboka and the Baby Monster."

Baada ya kurejea kutoka Winona, tulijiandaa kwenda Excelsior, kuhudhuria uzinduzi wa filamu ya "Papa's Shadow." Filamu hii inamhusu mwandishi Ernest Hemingway, na kwa kiasi kikubwa ni mazungumzo baina yangu na Mzee Patrick Hemingway, kuhusu maisha, uandishi, na fikra za Hemingway.

Matokeo ya mazungumzo yetu yalivyo katika filamu yamewasisimua sana watazamaji. Nilitegemea hivyo, kutokana na kwamba inaleta mtazamo mpya juu ya Hemingway.


Mtengenezaji wa filamu ni Jimmy Gildea, ambaye alikuwa mwanafunzi wangu katika kozi ya "Hemingway in East Africa," niliyofundisha Tanzania mwezi Januari mwaka 2013. Anaonekana pichani hapa kushoto akiwa nami na binti zangu.





Monday, June 22, 2015

Ernest Hemingway, a bridge between cultures

An excellent opportunity to learn why Ernest Hemingway fell in love with Cuba, was how Julián González, Cuban Minister of Culture, described the 15th International Colloquium dedicated to the author of The Old Man and the Sea, an academic event which began yesterday, June 18, in the presence of researchers and followers of the life and work of the great writer.
The Minister spoke to the press regarding the number of U.S. scholars who attend each edition of the event and how their interest in the life of the winner of the Nobel Prize for Literature also brings them closer to the social and cultural life of the island.

What made Hemingway fall in love with our country, he noted, were the characteristics of the people, as “he was an enemy of formalities and here he found a suitable setting for his work, without the usual protocol of other big capitals. This spontaneity is multiplied in the cultural level of our people, in the way that they appreciate the arts in general and literature in particular.”

He highlighted the role of Hemingway as a bridge between two cultures, “today more than ever because once Americans are able to travel to Cuba freely, a great incentive will be to discover what it was the writer found here, what he saw in our people that made him established himself here and take to Cuba as a second home.”

The opening day of the conference began with a tribute to René Villareal, Hemingway’s butler at his Finca Vigía home, and who the bestselling author called his Cuban son.
Villareal was the confidant of the famed writer for 14 years, but their relationship dated from his childhood, when in 1939 the Pulitzer Prize winner rented the property because in it he found the peace to write.

The tribute was followed by the presentation of the book, The Last Lion, by Argentine Professor Richard Koon, which in six parts takes a journey through the life of the remarkable writer from his childhood in Illinois until his death in Idaho.

Koon noted that the research for the book had taken some four decades and it brought together the testimonies of people who in various ways were linked to the life and work of Hemingway, including the Catalan artist Joan Miró and the writer Rafael Alberti.

The program for the coming days of the event, which ends Sunday, includes celebrations for the 80th anniversary of the first edition of Green Hills of Africa, and the 90th anniversary of the publication of his book of short stories In Our Time.

A panel entitled, Hemingway and Martha Gellhorn: In love and war, led by Professor Sandra Spanier, University of Pennsylvania, and the book launch of Hemingway: the unknown, by Cuban Enrique Cirules, will also feature.

Fotos con pies y créditos:
Ricardo Koon, author of the book The Last Lion. Photo: Padrón, Abel

Chanzo: Granma

El legado de Ernest Hemingway es celebrado en Cuba

La vigencia del célebre autor también está en las películas basadas en sus obras / El evento resaltó la vida y obra del Premio Nobel de Literatura


Caracas, 22 de junio de 2015.- Considerado el Dios de Bronce de la literatura norteamericana, expertos sostienen que la vigencia de sus obras no ha palidecido.

Este domingo culminó el XV Coloquio Internacional Ernest Hemingway realizado en Cuba, con la participación de expertos de diferentes partes del mundo. Un estudioso cubano participante del evento resaltó la vida y obra del Premio Nobel de Literatura y manifestó que la personalidad del célebre autor ha creado una serie de mitos, sitios y plazas en los lugares donde él vivió.

"La efigie de Hemingway (1899-1961) flota en un limbo, que va desde La Habana a Paris, Nueva York, España, Italia, el Caribe, desde Tanzania a Centroáfrica, y al parecer no va a desaparecer todavía" declaró un participante del Coloquio. En 1954, Hemingway le entregó la medalla del Premio Nobel a la Patrona de Cuba, La Virgen de la Caridad del Cobre, como reconocimiento al pueblo cubano, inspirador de su obra El viejo y el mar.

La vigencia de Hemingway también está en las películas basadas en sus obras, como “Adiós a las armas”, “Por quien doblan las campanas” y “Forajidos”, entre otras, que fueron interpretadas por prestigiosos actores y actrices. Una buena parte de la distensión entre Cuba y Estados Unidos está apoyada en las relaciones entorno a la vigencia de Hemingway en la Isla. MCM

VTV /TeleSur

(Chanzo: Venezolana de Televison)

Tangazo la Maongezi Yangu Books on Central, Faribault

Kwa miaka mingi, nimeongea na hadhira mbali mbali hasa kuhusu tofauti za tamaduni. Matangazo huandaliwa na kusambazwaa kabla ya mikutano. Ka...